Exploring the Bible - 16

Swahili

UNABII WA DANIELI

MUNGU WA MBINGUNI ATAUNDA UFALME.”

Somo la 16 Soma: Daniel 2

Daniel Nabii.

Wakati Yeremia alipokuwa anawaonya watu wake huko Yerusalemu kuwa Nebukadineza Mfalme mwenye nguvu wa Babiloni angerudi kuja kuteketeza Yerusalemu kwa sababu ya uovu wao, Danieli tayari alikuwa mateka wa Kiyahudi Babiloni. Alikuwa amepelekwa uhamishoni katika mapambano yaliyotangulia mwaka 606 kabla ya kristo na kuwekwa katika kundi la wateule la mateka wa kiyahudi ambao Nebukadineza alikuwa amechagua ili waelimishwe katika busara na utamaduni wa Babiloni (Danieli 1). Danieli alikaa huko kipindi chote cha miaka 70 ya utumwa ambacho Jeremiah alikuwa ametabiri, akipanda cheo na kufikia kiwango cha kujulikana katika ufalme kutokana na busara na msimamo wake (Danieli 6:28; Jeremiah 25:8-12)

 

Ndoto ya Nebukadineza (Danieli 2)

Katika sura ya pili ya kitabu cha Danieli tunasoma juu ya tukio muhimu. Nebukadineza aliota ndoto ambayo ilitibua sana akili yake. Aliona taswira ya mwanaume mkubwa ambaye kichwa chake kilikuwa dhahabu, kifua na mikono ya fedha, tumbo na mapaja ya mchanganyiko wa shaba na zinki, miguu ya chuma, nyayo zake zikiwa za mchanganyiko wa chuma na udongo. Halafu akaona jiwe likiiponda tawira hiyo miguuni kwa nguvu kiasi cha kuiangusha chini na kuvunjika vipande vipande. Jiwe lilikua na kuwa mlima mkubwa wa kujaza dunia nzima. Ndoto hiyo ilikuwa inaonekana wazi na taswira iling’aa na kutisha kwamba Nebukadineza alilazimika kutafuta tafsiri yake. Aliwaita wachawi na wataalamu wake wa nyota wamwambie ndoto ilikuwaje na maana yake, lakini pasipo shaka hawakuweza. Habari hiyo ilipomfikia Danieli alimwomba Mungu wake ambaye alimfunulia kuwa alikuwa ndoto yenyewe ilikuwa inaeleza mambo ambayo yangetokea “siku za baadaye” (Danieli 2:28). Huu ni mmoja tu kati ya nabii kadhaa katika Biblia ambazo zinaeleza mambo ya “siku za baadaye.”

Ndoto. (Danieli 2:28-45)

Danieli alianza kuieleza ile ndoto kwa usahili na tafsiri yake kama Mungu alivyokuwa amemfunulia. Picha ya kisanii ya taswira hiyo inaonyeshwa katika ukurasa ufuatao, pamoja na tafsiri ya Danieli na jinsi historia ilivyothibitisha undani wake.

Mungu wa mbinguni atasimika ufalme (Danieli 2:44)

Nguvu ya ile jiwe na kazi yake imeelezwa wazi wazi katika aya ya 44 na Danieli anaposema: “katika siku za hawa wafalme Mungu wa mbinguni atasimika ufalme ambao hautavunjwa kamwe: na ufalme na huo ufalme hautaachwa mikononi mwa watu wengine ila utavunja na kumaliza kabisa falme zote hizi na utasimama milele.

Angalia vidokezo hivi vya kupendeza katika aya ya 44

 

  1. Kwa wakati uliopangwa Mungu atasimika ufalme.

  2. Ufalme huu hautavunjwa (kama Babiloni na ufalme wa Umede na Ajemi ulivyovunjwa n.k)

  3. Utawala wa ufalme huu hautaachwa mikononi mwa watu. Yesu Kristo na wale wafuasi wake waaminifu ambao wamefanywa wasife, arudipo ndiye atakayetawala (Mathayo 25:34; Luka 19:17).

  4. Ufalme wa Mungu, ukiwa na Yesu Kristo kama mfalme utavunja mifumo mengine yote ya kisiasa.

  5. Ufalme wa Mungu utasimama milele (2Samueli 7:12-16; Luka 1:31-33)

 

Kwa hiyo katika ndoto hii ya kushangaza pamoja na tafsiri yake tunapata historia ya dunia tangu enzi za Nebukadineza hadi wakati yesu Kristo atakapotumwa na Mungu kusimika ufalme wake hapa duniani.

Huu ndiyo ufalme ambao Yesu aliwafundisha wafuasi wake kuomba aliposema “ufalme wako uje. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni” (Mathayo 6:10).

Pia tunasoma kuhusu wakati huu ambapo Yesu atatawala dunia: “Falme za dunia hii zimekuwa falme za bwana wetu na za Kristo wake na atatawala milele na milele” (Ufunuo 11:15).

Nabii Danieli mwenyewe alipewa maono kadhaa ambayo pia yanaonyesha historia ya dunia tangu mwaka 606 kabla ya Kristo hadi Ufalme wa Mungu utakapoanzishwa hapa duniani.

Mungu atawala katika ufalme wa watu.

Mojawapo ya masomo ya kimsingi na muhimu sana tunayojifunza katika unabii wa Danieli ni kwamba Mungu anadhibiti matukio ya duniani na anayaendesha kulingana na mpango aliokwishatuonyesha.

Danieli alimpendeza Nebukadineza kwa somo hili kiasi kwamba mfalme huyu mkuu mtawala wa ulimwengu wakati huo, alilazimika kutambua mamlaka ya Mungu wa Danieli “Na mwisho wa nyakati, mimi Nebukadineza niliinua macho yangu mbinguni, na uelewa wangu ukanirudia na nikambariki aliye juu kuliko wote, na nikamsifu na kumheshimu anayeishi milele ambaye milki yake haina mwisho, na ufalme wake ni wa kizazi hadi kizazi. Na wakazi wote wa dunia wanajulikana kwa kutokuwa kitu na anatenda jinsi atakavyo katika jeshi la mbinguni, na miongoni mwa wakazi wa duniani na hakuna hata mmoja awezaye kuzuia mkono wake au kusema, unafanya nini?” (Danieli 4:34-35)

Danieli alikuwa amemwambia kuwa “Aliye juu hutawala katika ufalme wa wanadamu, na humpa ufalme ampendaye na humpa ufalme mtu wa chini kuliko wote” (Danieli 4:17) Nebukadineza alikiri kuwa haya ndivyo yalivyo.

Ndoto ya Danieli – Mataifa yaonywesha kuwa wanyama (Danieli 7)

Danieli mwenyewe alipewa ndoto ya ajabu ambayo pia alitabiri urithisho wa himaya za dunia tangu wakati wake hadi hapo ufalme wa Mungu utakaposimikwa duniani. Ndoto na tafsiri yake ziko katika kitabu cha Danieli sura ya 7. Katika ndoto hii himaya nne za dunia zinazofuatana zinaonyeshwa kama ni wanyama. Hatujaachwa kushangaa hawa wanyama wanawakilisha kitu gani kwani Danieli aliuliza na kupewa jibu “Hawa wanyama wakuu ambao ni wanne, ni wafalme wanne ambao watainuka hapa duniani. Lakini watakatifu wa aliye juu zaidi watachukuwa ufalme na kumiliki ufalme milele na milele yote (Danieli 7:17-18). Tafsiri pana yatuambia kwa mara nyingine juu ya himaya nne za dunia ambazo nafasi zake zitachukuliwa na ufalme wa Mungu. Watakatifu ni wale watumishi waaminifu wa Mungu ambao watakuwa hai wakati Yesu anaporudi au watakaofufuliwa na kufanywa wasife tena. Kazi yao itakuwa ni kutawala na Yesu katika ufalme wa Mungu.

Wanyama wanne waliotajwa ni:-

  • Simba – akiwakilisha himaya ya Babiloni

  • Dubu – akiwakilisha himaya ya Mede ya Kiajemi

  • Chui – akiwakilisha himaya ya Kigiriki

  • Mnyama wa kutisha – akiwakilisha himaya ya Kirumi

Kila mnyama ana vitu vinavyomtofautisha ambavyo wanafunzi wa Biblia kwa muda wa miaka 1500 na zaidi wamevitambua kama za hizi himaya nne za dunia.

Mfano wa hili ni chui ambaye alikuwa na vichwa vinne na mbawa nne.

Historia inakumbusha kuwa baada ya kifo cha Aleksanda mkuu himaya ya Kigiriki iligawanyika katika sehemu nne kila mmoja akipewa mmojawapo wa majenerali wake wanne. Hili ni jibu la vichwa vine na mbawa nne. Kwa kuhusishwa na Mungu, Danieli alitabiri haya miaka 300 kabla hayajatukia.

Mnyama wa nne.

Swali linalofuata ambalo linakuja akilini mwetu ni: “Kama himaya ya Kirumi ilivunjwa mwaka 400 baada ya Kristo, tutapata wapi maelezo ya kuanzia wakati huo hadi sasa?” Kwa kweli Mungu ameisha yaonyesha kiwazi hasa.

Utaona kwamba mnyama alikuwa na mapembe manne, Danieli aliuliza haya yalikuwa na maana gani na aliambiwa: “Mapembe manne katika ufalme huu ni wafalme 10 watakaoinuliwa” (Danieli 7:24). Hapa pia tunatambulishwa kuvunjika kwa himaya ya Kirumi katika falme mbalimbali, na hicho ndicho historia inatuambia kilitukia Ulaya. Tuliliona hilo katika kitabu cha Danieli sura ya 2.

Halafu Danieli aliona “pembe lingine dogo” likitokeza miongoni mwa yale 10 na likawa kuu zaidi. Pembe hili lilikuwa na macho kama binadamu na mdomo ulionena maneno makuu” (aya ya 8). Pia tunapewa ishara za kutambua pembe hili ambalo lilijitokeza kwenye mnyama wa Kirumi. Ni utawala “uliopigana vita na watakatifu” (Wafuasi waaminifu wa Injili ya kweli ya Yesu Kristo na kuwashinda (aya ya 21) ikiwatesa wale wote waliokataa kukubali mamlaka na mafunzo yake. Pembe hili linawakilisha mfumo wa ki-dini unaodai kuwa na mamlaka ya kutoa amri za ki-dini, hata hivyo amri zake zinapinga ukweli wa neno la Mungu. Tunasoma: “Na atasema maneno makuu dhidi ya Aliye Juu zaidi na atawachosha watakatifu wa Aliye Juu zaidi na kuwaza kugeuza nyakati na sheria” (aya ya 25). Historia inazo kumbukumbu za dini hii iliyochoka ambayo imejitwalia maguvu ya kidini na kisiasa hasa katika eneo la himaya ya Ki-rumi ya zamani. Maelezo ya kina zaidi ya dini hii ya uongo ya Kikristo ambayo ilizuka yamo katika nabii za baadaye katika 2 Wathesalonike 2 na Ufunuo 13-19.

Kwa hiyo Mungu alimfunulia danieli mambo makuu ya kisiasa na ki-dini ambayo yamekuwepo tangu nyakati hizo hadi nyakati zetu, kwa mara nyingine tena historia inathibitisha unabii huu wa kushangaza.

Ufalme wake uje” – Ufalme utakuja

danieli alimalizia unabii huu pia na ahadi kwamba Mungu ataingilia kati mambo ya dunia na kuweka ufalme wake hapa duniani.

Tunasoma:

  • “Watakatifu wa aliye juu zaidi watachukua ufalme na kuumiliki milele na milele.” (aya ya 18)

  • “Mzee wa siku alikuja na hukumu ikatolewa kwa watakatifu wa aliye juu zaidi,na wakati ukafika ambapo watakatifu waliumiliki ufalme.” (aya ya 22)

  • “Na ufalme na utawala na ukuu wa falme zote chini ya mbingu yote watapewa watu wa watakatifu wa aliye juu zaidi ambaye ufalme wake ni ufalme usiokuwa na mwisho na tawala zote zitamtumikia na kumtii yeye. (aya ya 27)

hivyo katika nabii mbili hizi (Danieli 2 na 7) Danieli ametabiri kuwa kila mfumo wa kisiasa na mfumo wa dini ya uongo itafagiliwa mbali Yesu atakapokuja kuanzisha ufalme wa Mungu duniani. Tunapofikilia miaka 6000 ya giza la mateso iliyopita katika utawala wa mwanadamu tunashukuru kiasi gani kwamba Mungu ana udhibiti wa hali hiyo na karibuni atamtuma Yesu Kristo kuitawala dunia hii kwa haki (Mat-17:31)

Danieli atabiri matukio ya “nyakati za mwisho” (Danieli 11:40; 12:3)

Danieli siyo tu kwamba alitoa mtazamo mpana wa historia ya dunia hadi ufalme wa Mungu utakaposimikwa duniani bali pia alizungumzia matukio yatakayotokea karibu na kuanzishwa kwa ufalme huo. Alifunua kuwa “wakati wa mwisho” (aya ya 40) mamlaka ya kijeshi inayoitwa “mfalme wa kaskazini” atavamia mashariki ya kati kupitia Israel hadi Misri. Huu utawala wa kaskazini umetambuliwa na wasomi wengi kuwa ni shirikisho la mataifa likiongozwa na Urusi.

Angalia madokezo makuu:-

  • Matukio yatatokea wakati wa mwisho

  • Taifa lenye nguvu la kaskazini linaingia kijeshi mashariki ya kati likiwa na nia ya kuitawala Israeli na Misri (Danieli 11:40;43)

  • Taifa hili la kaskazini lenye nguvu linateketezwa Israeli (Danieli 11:44-45)

  • Yesu Kristo anarudi na wafu wanafufuliwa (Dan. 12:1-2)

  • Wenye haki wanapewa uzima wa milele ili kutawala pamoja na Kristo (Dan. 12:3)

Danieli 12:1-3 inaonyesha kuwa wakati ule ule uvamizi wa Israeli kutoka kaskazini unapofanyika (“yaani wakati wa mwisho”). Ufufuo wa wafu utakuwa unafanyika pia.

  • “Kutakuwa na wakati wa matata ambao haukupata kutokea tangu liwepo taifa hadi wakati huo.”

  • “Wakati huo watu wako watakombolewa , kila mmoja atakayekuwa ameandikwa kitabuni.”

  • “Wengi wanaolala ardhini wataamka.”

  • “Baadhi watapata uzima wa milele.”

  • “na baadhi watapata aibu na dharau ya milele.”

  • “Wale wneye busara watang’ara kama anga.”

  • “Wale wanaowaongoza wenzao katika haki, wataangaza kama nyota milele na milele.”

Mashariki ya kati sasa hivi ikiwa katika hali ya mvutano usiokwisha na mataifa mengi ya ulimwengu katika vurugu hakuna shaka kwamba tumo katika zile siku ambazo kwa wazi kabisa zinatangaza kuwa Yesu Kristo karibu atarudi kuja kuanzisha ufalme wa Mungu.

Nyongeza – “Siku za baadaye”

“Nabii za baadaye” katika Biblia ni za kupendeza kwa wanafunzi wa Biblia. Kwa hiyo tunatoa maoni machache kuhusu mojawapo ya nabii hizi iliyomo katika Ezekiel 38. hapa ya zote mbili, ya 8 na ya 16 zazungumzia matukio haya kama yalivyotokea “miaka ya baadaye” na “siku za baadaye” Unabii huu unahusiana sana na unabii wa Danieli kuhusu nyakati za mwisho (Dan 11:40-12:3) Ezekieli 38 yatuambia kuhusu muungano wa mataifa ya kijeshi mengiyayo yakitokea kaskazini ambayo yatakuja kuivamia Israeli “katika siku za baadaye.” Hatua hizi zitakunzwa na kundi lingine lenye nguvu lakini hatimaye Mungu ataingilia kati na matokeo yake ni kwamba watu wote wa dunia watamkiri na kumwogopa.

Muhtasari wa Ezekieli 38.

 

  • Matukio yaliyozungumzwa yatatokea “katika miaka au siku za baadaye” (aya ya 8, 16)

  • Kiini cha ugomvi uliotabiriwa kitakuwa nchi ya Israeli (aya ya 8, 18)

  • Wayahudi kwa kiasi watakuwa wamekusanyika tena na kujiimarisha katika nchi yao (aya ya 8, 12). Hili limetimizwa tangu 1948 wakati Israeli ilipokuwa taifa katika nchi yao baada ya takribani miaka 1900 ya mtawanyiko katika kila taifa la dunia.

  • Jeshi la kaskazini au “mwenyeji” (aya ya 15) litaongozwa na “Gog wan chi ya Magog” ambaye ni mwana wa mfalme wa Rosh na Tubal (aya ya 3) “Rosh” ametambuliwa na wasomi wengi kuwa Urusi (angalia kidokezo chini)

  • Taifa hili gomvi la kijeshi liataingia Israeli kutoka kaskazini na sehemu za kaskazini (aya ya 6, 15) usemi huu wa Ki-ebrania umetafsiriwa kwa namna tofauti tofauti; “sehemu za kaskazini ya mbali kabisa.” “sehemu za mbali sana za kasakazini na “……………………….

  • Kwa mara nyingine kusababisha watu wengi kuitambua urusi kuwa ndilo taifa chokozi.

  • Ulaya ndiyo itakayoshirikiana na Urusi (Magog, Gomer) na Asia magharibi ambayo ni Uajemi au Iran na Targamah au Armenia, Libya na Ethiopia (Uhabeshi) (aya ya 5-6). Tazama ramani inayoonyesha mataifa haya.

  • Uvamizi wa kaskazini utakunzwa na “Tarshish” na “samba wake watoto” (aya ya 13). Wasomi wengi wanatambua kuwa Tarshish ni Uingereza na Jumuia ya Madola pamoja na washiriki wake wa kibiashara kama Amerika.

  • Pia katika ushirika na Uingereza itakuwamo “Sheba” na “Dedan” (yaani Saudi Arabia na mataifa mengine ya ghuba ya Arabia).

  • Katika kilele cha mzozo huo Mungu ataonyesha uwezo uwezo wake mkuu (aya ya 18-19) wakati Yesu Kristo anapojionyesha katika dunia (Zekaria 14:1-5, 12:9-11)

  • Matokeo yake yatakuwa kwamba uwezo wa kijeshi wa Muungano huu wa kaskazini utateketezwa (Ezekiel 39: 3-5)

  • Mataifa yote yatafanywa yatambue kuwa Mungu wa Israeli ndiye aliyepata huu ushindi (Ezekieli 38:23; 39:7)

  • Hapo Israeli itatambua upofu wake wa siku za nyuma na kukubali njia ya Mungu na kumkiri Yesu Kristo kama mwana wa Mungu na mkombozi wao na mfalme (Ezekieli 39:7; 27:29; Waroma 11:25-26)

Angalia: Wasomi kwa karne nyingi wamelieleza neno chifu lililomo katika aya ya 2 ya Biblia ya Tafsiri mpya kwa hiyo sehemu ya sentensi husika inasomeka “mwana mfalme wa Rosh” (linganisha na Biblia mpya ya Amerika na Rotherham).

Rosh inatambuliwa kuwa jina la kale la Urusi na majina Meshech na Tubal yanafananishwa na sehemu fulani Fulani za Urusiwanahistoria maarufu kama Bochart na Rollin wanaunga mkono maoni haya, ambapo mwandika kamusi wa Kiebrania Gesenius amesema, katika kamusi yake 1847 chini ya neno “Rosh”.

Taifa la kaskazini lililotajwa pna Tubal na Meshech: bila shaka Warusi waliotajwa na waandishi wa Byzantini wa karne ya 10 chini ya neno “Ros.” Kwa sababu hizi wengi wanaamini kuwa taifa la kaskazini litajwalo hapa ni Urusi.

Muhtasari

  • Danieli alitafsiri ndoto muhimu ambayo Mungu alimpa Nebukadineza. Katika ndoto hii aliona historia yote ya dunia iongozayo kwenye kipindi ambacho Mungu wa mbinguni angesimika ufalme wake ambao hautavunjwa kamwe (Danieli 2:44)

  • Danieli alimueleza Nebukadineza kuwa “Yule aliye juu zaidi anatawala katika ufalme wa watu na humpa amtakaye” (Danieli 4:17). Hili linatuhakikishia kuwa Mungu ana udhibiti wa mambo ya kidunia na atatimiza mpango wake.

  • Tena Danieli aliambiwa kuwa “watakatifu wa aliye juu zaidi watauchukuwa ufalme na kuumiliki milele na milele (Danieli 7:18)

  • Historia imedhihirisha kikamilifu kuwa unabii wa Danieli umehusishwa na Mungu. Mtume Petro aliandika: “Kujua hili kwanza, kuwa hakuna unabii wa maandiko ambao ulio na tafsiri za kibinafsi. Kwa sababu unabii ulikuja zamani si kwa matakwa ya mwanadamu bali watu watakatifu wa Mungu walinena kadiri walivyoagizwa na Roho Takatifu.” (2 Petro 1:20-21)

  • Katika “wakati wa mwisho” taifa lenye nguvu kutoka kaskazini litaivamia Israeli na pale litateketezwa na kuingilia kati kwa Yesu Kristo (Danieli 11:40-45)

  • Wakati huo huo “kutakuwa na wakatiwa matata” duniani, “ambayo hayajapata kutokea tangu kuwepo kwa taifa.” Huu pia utakuwa wakati wa ufufuo wa wafu. Baadhi watapewa uzima milele na wengine watakataliwa (Danieli 12:1-3).

Maswali (somo la 16)

  1. Ni ndoto gani aliyoota Nebukadineza ambayo Danieli alitafsiri?

  2. Madini yale manne yaliwakilisha falme zipi?

  3. Danieli 2:44 inabashiri kitu gani?

  4. Tunajifunza nini katika Danieli 4:17?

  5. Danieli alisema “Watakatifu wa Mungu aliye juu zaidi” wangechukua ufalme na kuumiliki milele (Dan. 7:18)

  6. Danieli anafunua matukio ya “wakati wa mwisho” Ni yapi hayo?

  7. Ni kwa njia zipi unabii wa Ezekieli 38 unafanana na unabii wa Danieli 11:40-12:4?

 

DANIELI ATAFSIRI NDOTO (Dan. 2:28-45)

Kichwa cha Dhahabu

Hii ilimwakilisha Nebukadineza na ufalme wa Babylon (aya ya 37-38). Himaya hii hatimaye ilivunjwa na Medi Ajemi mnamo mwaka 538 k.k (Dan. 5:28)

Kifua cha Fedha

Himaya ya Mede Ajemi inaonyeshwa. Ilipindua Babylon lakini nayo ikapinduliwa na Alexanda Mkuu mwaka 334 k.k.

Tumbo na Mapaja ya Shaba na Zinki

Alexanda Mkuu alianzisha Himaya ya Kigiriki kwa kupindua Mede Ajemi. Himaya yake ilianza hadi Misri na mto Indus mashariki. Baada ya kifo chake eneo alilotawala liligawanywa ka majenerali wake wanne.

Miguu ya Chuma

Majeshi ya Kirumi yalizishinda zile sehemu nne za Himaya ya Kigiriki yakipanua sehemu magharibi hadi bahari ya Atlantiki. Hatimaye kulikuwa na sehemu ya magharibi nay a mashariki. Upande wa magharibi ulitawaliwa na Roma hadi 476 B.K. upande wa mashariki ulitawaliwa na Konstantinopo hadi 1453 B.K.

Nyayo – Mchanganyiko wa Chuma na Udongo

Himaya ya Kirumi ilivunjwa na kugawanywa na wavamizi mbalimbali kutoka kaskazini na mashariki k.v. Wavandali, Wagoth na Wahum. Hadi sasa hakujawa na taifa la kuziunganisha sehemu hizi za himaya zilizotangulia.

Jiwe

Jiwe linagonga na kuvunja sanamu hii na sehemu zake ‘pamoja’ danieli aliona kuwa katika “siku za baadaye” serikali zitakazokuwa zinatawala katika himaya hizi kongwe zitaungana katika muungano au ushirika na kwamba Mungu atavunjilia mbali muungano wao akibadili na ufalme wake utakaotawaliwa na Yesu Kristo. Jiwe litatanuka na kujaa katika dunia nzima.

 

 

Swahili Title
UNABII WA DANIELI
Swahili file
Status
Added to Internet
African text
Christadelphian Bible Mission
Translator 1
Raphael Mkeya
Literature type