Sura ya 3. Biblia sauti ya Mungu[1]
Uzi wa Dhahabu
Baada ya kusoma vitabu vinavyofanyia kazi kanuni za Biblia, msomaji atatambua upesi kwamba ujumbe ule ule unarudiwa mara nyingi kwa njia nyingi. Vitabu vya Biblia vinaungana ili kufunua kusudi la mwenyezi Mungu. Hakuna kitabu chenyewe kinachoonyesha picha nzima. Kwa pamoja tuna vipande vyote vya picha za mafumbo. Ni wajibu wa kila msimaji kusoma ili kuunganisha yote (Mithali 25:2). Kila kitabu cha Biblia kina ujumbe uleule lakini kinaongeza maelezo madogo madogo ambayo hayajatolewa na vitabu vingine. Umoja unaonyesha wazi kwamba vitabu vingi vinatoa ujumbe mmoja. Uiofumwa ndani ya muundo unaoendelea wa Biblia. Ni ujumbe kwamba Yahweh ana mpango na kusudi na uumbaji na kwamba anatafuta kuwaokoa wanadamu wanaoweza kufa kutokana na Dhambi. Kutokuoa huku kunatia muhuri uandikaji wa ujumbe kwa mamlaka ya pamoja na kwa tumaini lisilopatikana katika ulimwengu wa kale wa kusini, mwa ulimwengu.
Sehemu kubwa ya ulimwengu wa kale huonyesha Mungu hakupendezwa na mambo ya wanadamu. Biblia inamuonyesha Yahweh akiwa na mwanadamu katikati ya mpango wake na kusudi. Katika suala hili, Biblia ni ya kipekee kwa hati ya zama kama hizi. Hakuna Imani nyingine ya wakati huu iliyo na tumaini la kutokufa kwa mwanadamu wa kawaida. Hata mfumo wa Imani wa Wamisri uliona kutokufa kuwa ni kitu tu kwa firauni ambao walikua miungu duniani tayari. Biblia inatoa tumaini kwa mwanadamu wa kawaida. Kichwa cha kusoma neno la Mungu kutoa Imani na kusababisha tumaini ni uzi wa dhahabu unaoenea katika kila kitabu cha kanuni.
Kama mwandishi wa hapo awali alivyosema kwa kufaa sana “Hapa kuna kitabu kilichoandikwa na waandishi arobaini wanaoishi katika zama tofauti bila tamasha au njama inayowezekana. Kujitokeza katika kitabu ambacho katika sehemu zake zote kimetawaliwa na Roho moja, fundisho moja na namna moja na kwa mamlaka ya anga kuu ambayo ni tabia yake ya kipekee. Kitabu kama hicho ni muujiza wa kifasihi. Haiwezekani kuhesabu uwepo wake kwa kanuni za kawaida.” (Christendom Astray, Robert Roberts).
Kati ya vitabu sitini na sita tulivyo navyo kuna umoja ambao haungepatikana ikiwa waandishi hawangekuwa mwandishi mmoja anayedaiwa – mbunifu anayejua yote, Mungu ambaye anapendezwa sana na uumbaji wake. Huu ndio msingi wa tumaini la ndugu katika Kristo. Ni kwa kusoma Biblia tu ndipo tunaweza kukuza Imani inayohitajika kwa tumaini kama hilo “Basi Imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Mungu” (Warumi 10:17).
Katika kusikia kuna kitu Zaidi ya usomaji wa neno. Tunahitaji akoe neno linalotumika kwa usikivu wa ndani wa kiroho unaoambatana na kupokea Imani kutoka kwa Mungu.
Huko ni kutambua sauti ya Mungu.
“Hili tu ndilo nataka kujifunza kwenu, Mlimpokea Roho kwa matendo ya Sheria au kwa kusikia kwa Imani?” (Wagalatia 3:2)
“Basi yeye awapae ninyi Roho na kutenda miujiza kati yenu, anafanya hivyo kwa matendo ya sharia au kwa kusikia kwa Imani?” (Wagalatia 3:5)
Imani na kuamini katika Kanuni za Biblia hazitakuja kwa kusoma tu. Ukweli wa kile inachosema lazima uzungumzwe na kuonyeshwa ili kuleta Imani. Jinsi gani mhudumu wa neno la Mungu anaonyesha ukweli wa neno la Mungu kwa wale wa kusini mwa ulimwengu? Njia pekee ambayo nimepata ni kwa kuonyesha kupitia matendo ya kibinafsi kwamba mhudumu mwenyewe anaamini katika kile kilichoandikwa na kuwasiliana wakati matukio yanayotokea yanaonyesha ukweli wa kile ambacho Mungu ameandika. Tunapoona unabii wa Biblia ukitimizwa tunazungumza na wale wanaotuzunguka kuhusu utimizo wa unabii huo uliotimia. Tunapoona uzuri swa ua tunazungumza juu ya mkono wa uumbaji wa Mungu. Tunapoona upendo tunamshukuru Mungu kwa mema yaliyofanywa, utii wa kibinafsi kwa amri na maagizo huzungumzwa kwa sauti kubwa (kama sio sauti kubwa) kama neno linavyofanya. Onyo! Tendo moja la kutotii kwa mfanyakazi wa shambani linaweza kusababisha kutaniko zima kupoteza Imani yao. Kwa kusema kwa uhuru juu ya Neno tunawatia moyo wengine, kutafakari neno lazima (Zaburi 119:97) na tunathibitisha Neno (1Thesolanike 5:21), “Kulihubiri neno kuwa mara moja katika msimu nje ya msimu, karipia, kemea na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho” (2 Timotheo 4:2).
Muujiza wa ufunuo
Kuytamka Biblia kuwa muujiza wa kifasihi unaotegemea tu ujumbe wake uliounganishwa kungeshusha thamani ya kimuujiza. Kuna viashiria vingi vya Biblia yenye nguvu Zaidi ya Kibinadamu, si haba utimizo wa unabii. Hili ndilo jambo la msingi kwangu. Wanaume hutumia mbinu kama vile kuchungulia na kutengeneza katuni ili kujaribu kubainisha sayansi ya siku za usoni, hutumia satelaiti na ala za kisayansi. Kuna tofauti ndogo sana, hawezi kutabiri wakati ujao kwa kiwango chochote cha usahihi na angalau ya wakati ujao wa mbali. Mujngu wa Biblia yupo katika mwelekeo mzima wa wakati wote kwa wakati mmoja “Na ahimidiwe Bwana Mungu swa Israeli, tangu milele hata milele” (Mambo Ya nyakati 16:36, ESV). Mungu wa Biblia anaweza kutabiri matukio ya Mbali sana kwa sababu yeye yuko tayari na ameyaona yakitokea. Sifa hii ya kutatanisha iliyothibitishwa ya Mungu ni ushahidi wa kuwepo kwake na kutegemewa kwa neno lake. “Niulizeni habari ya maombi yajayo” alisema Mungu kupitia nabii Isaya “mimi ni Mungu wala hapana mmoja kama mimi nihubiriye tangu mwanzo na mwisho na tangu zama za kale mambo ambayo hayajafanyika bado” (Isaya 45:11,46:9-11).
Hata wakosaji wakubwa wa Biblia hawawezi kukataa kwamba Agano la kale lilikuwepo mda mrefu kabla ya kuzaliwa kwa Kristo. Bado maandishi ya musa ya watunga Zaburi na manabii yana Utabiri wa kina Zaidi kwa maisha na kazi ya Yesu. Angalia tu kwa mfano katika Mwanzo 3:15 na hasa katika Zaburi 22 na Isaya 53. Marejeo haya yanazungumza bila shaka juu ya Bwana Yesu Kristo. Kasha jiulize kwa unyoofu jinsi unavyoweza kueleza mbali uhakika wa kwamba unabii huo uliowazi juu ya Yesu ulikuja kuwa katika maandiko matakatifu ya Wayahudi. Wayahudi hao hao hawaamini kwamba kuna mwokozi. Wayahudi watakapoonyeshwa aya hizi watakuwa na aibu sana. Kwa mtindo kama huo inawezekana kuonyeha kwamba historia inayojitokeza ya Wayahudi na hatima ya mataifa mashuhuri ya ulimwengu iliainishwa na Mungu wa Biblia muda mrefu kabla ya kutokea kwa unabii wenye maelezo ya ajabu kabisa (Kumbukumbu la torati 28 Ezekieli 26 na Daniel 2 ni mkifano mkitatu tu kati yha mingi). Unabii kama huo ndio haswa tunapaswa kutarajia kutoka kwa akili ya Mungu anayejua yote ambaye huona historia nzima ya mwanadsmu kwa Dakika moja. Huu ni uthibitisho wa wazi wa tabia ya muujiza swa kweli ya usemi wa Biblia. Ni kiumbe tu mgeni kabisa kwa chechote tunachojua ndiye angeweza kuandika maneno haya.
Kusimulia wakati ujao wa Biblia unapotafsiriwa kwa usahihi ni kwa asili yake kuwa ni muujiza. Unabii Wa Biblia ni tofauti sana na Unabii wa Nostradamus au Sharman. Imefafanuliwa kwa urahisi na maandiko yenyewe. Haina utata. Daima hutokea kwa au bila kujaribu kuingiliwa na wanadamu. Hakuna Unabii ulioshindwa katika Biblia.
Kama ufunuo wowote wa muujiza unausisha matumizi ya nguvu za Mungu, roho weake mtakatifu. Kiwango hiki cha maelezo si cha kawaida haikuweza kupatikana kwa njia ya kuyeyuka, nguvu za giza au kiasi chechote cha kutafakari. Hili si jambo linaloweza kufikiriwa na wanadamu bila msaada wa Mungu. Biblia inaonyesha sifa zote za muujiza aombao waandishi wake wanatukumbusha mara kwa mara kwamba wao walikua vyombo vya mungu na si waanzilishi wa ujumbe “Watu watakatifu wa mungu walinena wakiongozwa na roho mtakatifu” anaeleza Mtume Petro (2 Petro 1:21) na hata Bwana Yesu mwenyewe alikiri kwamba yeye pia amekuwa mhusika wa kazi hii ya miujiza ya Mungu. “Kwa maana sikunena kwa nafsi yangu; lakini Baba aliyenituma ameniamuru niseme nini na niongee nini” (Yohana 12:49).
Muujiza huu unaelezwa kama msukumo katika Biblia. Inaweza kuonekana katika kurasa zote za kitabu. Iwe kupitia maono ya manabii, mitume au wajumbe wa malaika, Roho wa Mungu anaonyweshwa kama nguvu inayoongoza ujumbe. Biblia ina mengi ya kutuambia ambayo kama wanadamu tusingejua. Ni muujiza wa unabii ambao huleta ulimwengu wa miliki ya Mungu katika uwanja wa ufahamu wa mwanadanu. Biblia ni neno la mungu lililoandikwa kwa chapa.
“kila mtu kwa lugha yake”
Wakati muujiza wa lugha ulipowawezesha wale maelfu ya Wayahudi kutoka katika ulimwengu wote wa Kirumi ambao walielewa lugha za kigeni tu kuelewa injili ambayo mitume walikuwa wakihubiri siku ya Pentekoste (Matendo 2:1-11), ilikua ni ishara kwamba kile kilichofundishwa Mitume walitoka kwa Mungu.
Vile vile mtume Paulo ambaye Utume wake kama mtume kwa mataifa nje ya Yudea (Matendo 9:15) alikuwa na karama isiyo ya kawaida na uwezo wa kuhubiri katika Lugha nyingi (Wakorintho 14:18).
Muujiza sawa ulikuwa mi ewakati wa “utimilifu” (Wagalatia 4:4). Muujiza wa aina tatu. Ndugu Carter aliandika “inajulikana sana kwamba hakuna wakati wowote katika historia yake ulimwengu ulipotayarishwa kwa ajili ya kutangaza injili kama ilivyokua katika karne ya kwanza BK. Ilikua utimilifu wa wakati na matayarisho yalikua matatu. Kwanza kulikuwa na maandalizi ya kidini yaliyounganishwa na Taifa la Israel… pili kulikuwa na utayarishaji wa lugha na hili liliunganishwa na taifa la Kigiriki… mwishowe kulikuwa na maandalizi ya kisiasa yaliyounganishwa na Roma.” (Waefeso ch.1, John Carter)
Hivi vyote ni vielelezo vya wazi vya daraka muhimu ambalo tafsiri ya neno la mungu katika lugha za kigeni ingepaswa kutekeleza katika miaka ya baadaye katika kueneza uvutano wayo katika maisha ya mamkilioni ambao hawakuweza kuelewa Kiaramu cha awali cha Kiebrania na Kigiriki ambamo manabii wa Mungu na mitume waliongowa kunena na kuandika.
Lugha ya Kiingereza na miliki ya Uingereza katika siku hizi za mwisho zimekuwa na madaraka sawa na lile la lugjha ya Kigiriki katika wakati wa miliki ya Kirumi.
Maandishi yaliyopuliziwa hayahiotaji mwandishi aliyepuliziwa ili maana yake ifahamishwe kwa usahihi katika lugha nyingine. Mara tu maandishi ya Biblia yalipokamilika na mitume wenye Karama ya Roho “Wamelalla katika bwana” ilikuwa ni lazima tu kwamba Biblia ihifadhiwe kwa ajili ya Vizazi vilivyofuata ili kusoma au kutafsiri kwa wengine pia.
Ujuzi wa lugha na uwezo wa kuzitafsiri ni ustadi unaoweza kufundishika. Ingawa wewngi wa asili wanazungumza lugha ya kikabila, wengi pia watakua wamejifunza Kiswahili au Kiingereza kama lugha za Sekondari. Hakuna hata mmoja ambaye angesema katika kujifunza lugha hizi kwamba waliongozwa katika kufanya hivyo kwa njia yoyote ya kimiujiza. Wengi watakua wamejifunza lugha hizi karibu na moto kama zilivyofundishwa na wazee. Hata hivyo historia ya Tafsiri za Biblia kutoka toleo la Septuagint ya Kigiriki ya agano la kale la Kiebrfania katika karne ya tatu Kabla ya Kristo hadi tafsiri za Kiswahili za karne yetu ya ishirini, ni ushuhuda wa majaliwa ya Mungu katika kuwasaidia wanadamu kujifunza na kutumia ujuzi wao wa kibinadamu vizuri sana.
Historia za maisha za wanazuoni wakubwa kama John Wycliffe (1320-1384) na Williama Tyndale (1494-1536) zote zina maana za kuingilia kwa Mungu. kwa kujitolea kwao na usomi wao waliweza kutafsiri kwa Kiingereza mawazo ya mungu ambayo yalikua yamefichwa kutoka kwa watu wa kawaida katika Kilatini na mateso ya ukatoliki. Mateso ya kunyimwea haki ambayo hayakuweza kazi ya bidii ya watu kama hao isienwze uelewaji wa neno la Mungu kwa upana Zaidi kuliko wakati mwingine wowote.
Kuja kwa uchapajio wa herufu zinazoweza kusongeshwa (1454) labda uvumbuzi mkubwa Zaidi na wa kiteknolojia uliofikia mbali Zaidi kwa wakati wote ulikuwa pia kichocheo kwa wengine wengi waliozifuata, ilifanya Biblia ipatikane kwa kadri ambavyo haikuwaziwa hapo awali na ikisaidia kutimiza nia ya Tyndale ya kufanya hata mkulima mnyenyekevu aijue Biblia.
Ukuaji wa ghafla wa idadi ya nakala za Biblia zilizokuwepo ulikuwa wa ajabu sana katika karne ya kumi na tano na kumi na sita. Na tafsiri iliyoagizwa na mfalme James wa kwanza (ile inayoitwa toleo lililoidhinishwa) ilichapishwa mwaka wa 1611, ufundi wa kuchapisha toleo la mwanzo kwa vyombo vya habari na ustadi wa mtafsiri uliwekwa pamoja kwa njia ya uangalizi ili kuupa ulimwengu unaozungumza Kiingereza toleo la Biblia ambalo halijawahi kuzidiwa kwa mtindo na ubora. Toleo lililoidhinishwa ni ukumbusho wa majaliwa ya Mungu.
Kkingereza ndiyo lugha inayozungumzwa Zaidi duniani katika zama zetu hizi kwasababu Milki ya Uingereza ilitawala dunia hadi mda mfupi uliopita. Kuidhinisha biblia ya Kiingereza ilichukuliwa kuwa msingi wa maandiko matakatifu na mwaka 1997, ilichapishwa toleo la kwanza la biblia la Kiswahili. Tangu wakati huo matoleo mengi ya lugha za kikabila yalitolewa. Kupitia Ustadi wa mtafsiri, neno lililopuliziwa la mitume na manabii “limeenea katika Dunia yote na maneno yao hata mwisho wa dunia”. “Hakuna usemi wa lugha ambayo sauti yao haisikiki” (Zaburi 19:4, iliyonukuliwa katika Warumi 10:18).
Wakati ule ule ambapo Biblia ya kwanza ya Kiswahili ilichapishwea na jumuiya ya Biblia. Mtandao na simu ya mkononi vilivumbuliwa. “wakati wa mwisho maarifa yataongezeka” (Daniel 12:4). Bila shaka uvumbuzi huu umeleta mapinduzi makubwa sana katika kupatikana kwa Biblia kama vile aina ya kusonga mbele, mwaka wa 1454. Sio tu kwamba Biblia sasa inapatikana katika maduka ya Vitabu, lakini watu wengi katika sayari pia wana nakala mfukoni. Nyuma ya uzushi huu tunaweza kuona mkono unaoendelea wa mwenyezi Mungu ukitoa Riziki kiasi kwamba hakuna anayeweza kukataa kwamba wana uwezo wa kulifikia neno lake.
Dai lenye changamoto
Biblia inakuja mbele yetu kasha ikidai kusikilizwa kama neno la Mungu “Bwana asema hivi” na vishazi kama hivyo ni sehemu mujhimu ya maandishi ya Agano la kale. Kuondoa sehemu hizo zote za maandiko zinazodai msukumo wa Mungu kwa ajili yao wenyewe au kutambua kwa wengine kungeondoka lakini kubaki kidogo. Madai ya mtume Petro kwamba maandiko ya kiyahudi yalitolewa wakati “watu watakatifu wa mungu waliponena wakiongozwa na Roho mtakatifu” ( 2 Petro1:21) ni kweli au uwongo. Lakini tunapotambua ni kwa kiwango gani Bwana Yesu Kristo mwenyewe na mitume wake walitambua hilo Agano la kale kuwa neno la Mungu lenye mamlaka, haipaswi kuwa na shaka kwamba mtazamo wa mfuasi wa kweli wa Kristo unapaswa kuwa ule ule. “je soma”; “imeandikwa”; “maandiko yasemaje”. Hii ilikuwa misemo aliyoipenda Sana mwalimu aliporejelea sehemu kubwa Zaidi ya kile tunachojua sasa kama Biblia. Kwa kufanya hivyo Biblia inakua msingi wa yote tunayofundisha. Hapa ndipo mahali petu pa kuanzia kuelewa na kufundisha “ibilisi na Shetani” ufahamu wa pamoja wea maandiko ya kweli.
Muhimu pia Bwana Yesu alidai sin chini ya mamlaka ambayo vuviwa kwa maneno yake mwenyewe (ona Yohana 17:8) aliwaahidi mitume wake kwamba wao pia wangeongozwa kwa njia isiyo ya kawaida na roho mtakatifu, (Yohana 14:26,:15:26-27; 16:13-15) na Wakristo wa mapema wa Biblia walilichukulia kama fundisho la msingi kwamba “maandiko yote, (Agano la kale na Agano Jipya kufikia wakati huo) yametolewa na mungu na yanafaa” (2 Timotheo 3:16).
Madai hayo yenye changamoto ya Biblia juu yake yenyewe hayaachi njia ya kati kwa mwitikio wetu Binafsi kwa ujumbe wake. Ni lazima tukubali au tukatae. Kwa maana ikiwa dai hilo ni la uwongo basi ujumbe wa Biblia hauna thamani wa kweli na injili ya wokovu ilitomo ndani yake ni Hadithi tu ya mwanzo ya mwanadamu. Lakini ikiwa dai hilo ni la kweli basi ujumbe wa Biblia unaamuru utii na injili yake inatoa tumaini nje ya kaburi. Madai ya Biblia sio mazooezi ya kitaalamu bali ni suala la maisha na kifo.
[1] Sura hii inategemea kabisa kijitabu cha ndugu katika Kristo kiitwacho Muujiza wa Biblia Neno la Mungu Lililochapishwa na Reg Carr chenye mabadiliko machache na nyongeza ndogo.