Sura ya 6. Imani ya Mungu mmoja

Swahili
Sura ya 6. Imani ya Mungu mmoja

Sura ya 6. Imani ya Mungu mmoja[1]

Mungu peke yake

Mungu wa Biblia kama aliye mkuu wa Imani nyingi za kimapokeo na tofauti na jumuiya ya Wakristo kwa ujumla ni asiyeweza kufa na mwenye uwezo wote kwa wote. “Sasa kwa mfalme wa milele asiyeweza kufa, mungu wa pekee mwenye hekima iwe hekima na utukufu  milele na milele Amina” (1 Timotheo 1:17). Hakuna aliye mkuu kuliko yeye  “Baba yangu aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote” (Yohana 10:29). Kwa maana kamili anaanza kidogo,  mwisho kidogo. “na ahimidiwe Bwana wa Israeli, tangu milele hata Milele” (Zaburi 106:48). Mda na nafasi kidogo. Nguvu zake hazina kipimo, kwa kadri ambayo yeye ni nguvu (πνεῦμα pneuma strong g4151 pumzi, roho, akili, kufikiri nishati hai) “Mungu ni Roho” (Yohana 4:24) na alifanywa kuwa na nguvu na kuvifanya vitu vyote kutoka kwake “ roho ya Mungu I katika Pua yangu” (Ayubu 27:3).

Akili ya mwanadamu imnaona ni vigumu sana kufahamu umilele. Tunaweza kuelewa kwa urahisi kuishi milele kutokana na hatua hii ya wakati, tunaona ni vigumu Zaidi kuelewa kitu ambacho kilikuwepo siku zote. Hii ni kwasababu ya ubinadamu wakati unasafiri katiksa melekeo mmoja tu. Mara nyingi tunasikia swali “ni nini kilimfanya Mungu” au “Mungu alitoka wapi”?. Lakini Mungu amekuwepo siku zote. Dhana hii daima hupiga akili kupita kwa wakati hakuna maana katika muktadha wa Mungu “siku moja kwa Bwana ni kama miaka Elfu na miaka Elfu kama siku moja” (2 Petro 3:8).

Kuanzia kitabu cha kwanza hadi cha mwisho, Biblia inatuambia  kwamba Mungu ni Mungu mmoja na hakuna Miungu mingine ila yeye. Je yuko Mungu Zaidi yangu, hakuna Mungu; mimi simjui mtu yeyote” (Isaya 44:8).

Maelfu ya miaka iliyopita  mungu alizungumza na Israel kupitia Musa  mtu aliyewaongoza kutoka Misri.

Sikia Israel, Bwana Mungu wetu, ndiye Bwana mmoja, nawe mpende Bwana mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote na kwa nguvu zako zote” (Kumbukumbu la Torati 6:4-5).

Badae Mfalme Daudi wa Israel aliandika:

Ee Bwana, hakuna kama wewe, wala hakuna Mungu mwingine ila wewe, kama tulivyosikia kwa masikio yetu” (1 Mambo ya nyakati 17:20).

Mungu akizungumza kupitia Nabii Isaya alisema;

“Ninyi ni mashahidi wanguasema BWANA, na mtumishi niliyemchagua mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwepo mwigine” (Isaya 43:10).

“Kwa maana Bwana aliyeziumba mbingu, ndiye Mungu aliyeiumba Dunia, aliyeifanya imara asiyeiumba bure, aliyeiumba ili ikaliwe, asema hivi; Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine” (Isaya 45:18).

Tunapokuja kwenye Agano jipya tunakuta ujumbe ule ule ukirudiwa tena ukituambia kwamba Mungu ni mmoja. Mtume Paulo alisema:

“Lakini kwetu sisi Mungu ni mmoja tu, aliye Baba, ambaye vitu vyote vimetoka kwake, nasi tunaishi kwake; yuko na Bwana mmoja, Yesu Kristo, ambaye kwake vitu vyote vimekuwepo, na sisi kwa yeye huyo” (1 Wakorintho 8:6)

“Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja, Mungu mmoja na Baba wa wote aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya ninyi nyote” (Waefeso 4:5-6)

Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, mwanadamu Kristo Yesu” (1Timotheo 2:5).

Kuna mistari mingine mingi katika Biblia inayotuambia kwamba Mungu ndiye Mungu wa pekee wa kweli na kwamba hakuna miungu mingine isipokuwa yeye.

Kwa orodha Zaidi ya marejeleo zingatia yafuatayo:

Mungu ni mmoja

Ayubu 31:15; Zekaria 14:9; Malaki 2:10; Mathayo 2:17;23:9; Marko 2:7; 10:18; 12:29,32; Luka 18:19; Yohana 8:41; Warumi 3:30; 1 Wakorintho 8:4,6; Wagalatia 3:20; Waefeso 4:6; 1 Timotheo 2:5; Yakobo 2:19, 4:12.

BWANA (Yahwe) ndiye Mungu wa pekee wakweli

Kutoka 8:10, 9:14, Kumbu kumbu la Torati 4:35-39, 7:9, 32:12-40; 1 Samweli 2:2; 2 Samweli 7:22, 22:32; 1 Wafalme 8:23,39,60; 18:17-39; 2 Wafalme 5:15, 19:15-19; 1 Mambo ya nyakati 16:25-26; 2 Mambo ya nyakati 6:14, 13:9; Nehemia 9:6; Ayubu 9:8; Zaburi 18:31, 62:2,5-6, 71:16,19, 72:18, 73,25, 83:18, 86:8-10, 89:6-11, 90:1-2, 96:4-5, 118:27; 136:4, 148:13; Isaya 37:16-20, 40:18-25, 41:4, 43:10-13, 44:6-8,24, 45:5-7,14,18,21-22, 46:9; Yeremia 3:11, 5:7, 10:6-16, 16:20; Hosea 13:4; Yoel 2:27; Marko 12:32; Yohana13:16, 14:28, 17:3; Matendo 19:26; Warumi 16:27; 1 Wakorintho 8:4-6, 10:20; Wagalatia 4:8; 1 Timotheo 1:17, 2:5, 6:15-16; 1 Yohana 5:20; Yuda 25; Ufunuo 15:4.

Baba pekee ndiye Mungu mmoja wa kweli

Kumbu kumbu la Torati 32:6; 2 Samweli 7:8-14; 1 Mambo ya nyakati 17:11-14, 29:10: Zaburi 2:7, 89:26-29; Isaya 42:1, 61:1-2, 63:16, 64:8; Yeremia 3:4,19, 31:9; Malaki 1:6, 2:10; Mathayo 11:25, 24:36; Marko 10:18, 13:32; Luka 10:21, 18:19; Yohana 1:18, 5:43-44, 6:27,45, 8:41-42, 54, 14:28, 17:1-3, 20:17; Matendo 7:55-56; Warumi 1:7, 15:6; 1 Wakorintho 1:3, 8:6, 11:3, 15:24; 2 Wakorintho 1: 2-3, 11:31; Wagalatia 1:1-5; Waefeso 1:2-3,17, 4:5-6, 5:20, 6:23; Wafilipi 1:2, 2:11, 4:20; Wakolosai 1: 2-3, 3:17; 1 Wathesolanike 1:1-3, 3:11, 13; 2 Wathesolanike 1:1-2, 2:16: 1 Timotheo 1:2; 2 Timotheo 1:2; Tito 1:4; Filemon 3: Waebrania 12:7; Yakobo 1:27, 3:9; 1 Petro 1:2-3; 2 Petro 1:17; 2 Yohana3,9; Yuda 1: Ufunuo 1:6.

BWANA Mungu (Baba) ni mwenyezi na mkuu

Mwanzo 18:25; Kutoka 20:3-5, 22:20; Kumbu kumbu la Torati 10:17; Yoshua 3:11,13, 22:22; 1 Samweli 7:3-4; 1 Wafalme 18:17-39; 1 Mambo ya nyakati 29:11; Zaburi 47:2,7, 83:18, 97:9, 110:1, 136:1-26; Isaya 2:11,17, 26:13-14, 44:24; Danieli 2:47, 3:29, 11:36; Zakaria 6:5, Mathayo 4:10, 24:36, Marko 5:7, Luka 4:8, 8:28, Yohana 5:44; Matendo 7:48, 16:17; Warumi 16:27; 1 Wakorintho 3:23, 11:3, 15:24-28; 2 Wakorintho 6:18; Waefeso 3:14, 4:6; 1 Timotheo 1:17, 6:14-16; Waebrania 7:1; Yuda 25; Ufunuo 1:8, 4:8, 11:17, 15: 3-4, 16:7, 14, 19:6, 15, 21:22.

Baba wa ulimwengu wote ni Mungu wa viumbe vyote, chanzo cha kwanza na kiini cha vitu vyote  na viumbe. Kwanza fikiria Mungu kama muumbaji kasha kama mtawala na mwisho kama mtegemezi asiye na kikomo.

Wewe ndiwe BWANA, wewe peke yako; wewe ulifanaya mbingu, mbingu za mbingu, pamoja na jeshi lake lote, dunia na vyote vilivyomo baharini, na vitu vyote vilivyomo, wewe unavihifadhi vitu hivi vyote, na jeshi la Mbinguni lakusujudu wewe” (Nehemia 9:6).

Wazo la Baba wa ulimwengu mzima - Mungu mmoja lazima abadilishe akilini mwa mwanadamu, miungu mingi ya utandawazi wa kusini, na utatu wa jumuiya ya Wakristo ili kumwezesha mwanadamu anayeweza kufa kufahamu Mungu wa Biblia kama Baba kama muumba  wa kiungu na mtawala asiye na kikomo.

Mungu ndiye chanzo cha ukweli[2]. Mungu hufunika kote katika ulimwengu wa  nyenzo. Yeye ndiye chanzo cha kwanza na kitovu[3] cha ukweli wa milele.

Viumbe wanaokufa hupitia Msukumo usiozuilika wa kuashiria zana zao zenye kikomo za Mungu. Hawezi kufikiriwa kama mwanadamu, kama mashine, au kiumbe halisi. Yeye ni mbali Zaidi; Yeye ndiye chanzo cha kwanza.

 

 

[1] Sura hii inategemea kabisa kijitabu  cha Ndugu katika Kristo kiitwacho mungu mmoja au  Utatu J na D flint, chenye mabadiliko machache  na nyongeza ndogo

[2] Ufafanuzi wa kweli katika “kamusi ya Biblia ya Harper” inajumuisha usemi kwamba “Mungu ni kweli”.

[3] Kurejelea kwa makusudi maandishi ya mfumo wa Imani ya Urantina.

Swahili Title
Sura ya 6. Imani ya Mungu mmoja
Translator 1
Emanuel
Literature type