CSSA 2-2-03 - REBELLION IN ISRAEL

Swahili

153. UASI KATIKA ISRAEL

“Fimbo ya mtu nitakayemchagua itachanua”

Kwa kuzuiliwa kuingia Nchi ya Ahadi, wana wa Israeli walihukumiwa kutangatanga jangwani kwa miaka 38 (miaka 40 tangu kuondoka Misri) hadi kizazi chote kilichotangulia kilipongamizwa, isipokuwa Kalebu na Yoshua n.k. (Kumb. 2:14). Lakini, Yahwe hakuwaacha kabisa. Aliendelea kuwasiliana nao kupitia Musa (Hesabu 15:1, 17, 35). Alitoa mana kila siku, akawapa watu maji, na kuandaa mavazi (Kumb. 8:2-6; 29:5-6).

Wakati huohuo, watu kukatishwa tamaa, watu kushindwa - kila walipojaribu kuingia kwa nguvu katika Nchi ya Ahadi (Hesabu 14:45), hali ya jumla ya manung'uniko na hali ya kusumbuliwa kwa taifa,yakawa ni chanzo cha kuchochea hali ya kutoridhika. Fursa hiyo ilitumiwa na Kora kuendeleza madai yake. Alikuwa ni Mlawi mashuhuri, binamu wa kwanza wa Musa na Haruni (Kutoka 6:18, 21), na, kulingana na Josephus, alikuwa pia tajiri na msemaji mzuri. Alikusanya wengine karibu naye na kusema vibaya dhidi ya Musa na Haruni. Lakini, ukuhani ulitokana na kuteuliwa na Mungu, na tunaonyeshwa katika somo hili kanuni ya uteuzi wa kiungu.

Hesabu 16 & 17 (ona pia Kumb. 11:6-8); Zaburi 106:16-18

UASI KATIKA ISRAELI

Kora, kiongozi mashuhuri na binamu wa Musa na Haruni aliwaonea wivu viongozi hao wawili (Tazama Zaburi 106:16). Aliwakusanya Walawi wengine pamoja naye, na wakuu 250 “maarufu katika kutaniko” (m. 1-2), aliwapinga Musa na Haruni kwa shutuma kwamba walijichukulia kupita kiasi. Walidai kwamba, Israeli wote walikuwa watakatifu, na kwamba hapakuwa na sababu ya Musa na Haruni kujiweka juu ya wengine. Ni wazi kabisa Kora alitaka uongozi kwa ajili yake mwenyewe.

Musa alihuzunishwa sana na matendo hayo, lakini aliwaambia watu kwa ujasiri kwamba Mungu angeonyesha ni nani waliokuwa viongozi wake (mst. 5). Wale wakuu 250 kama walivyoamriwa, walikuja kwenye hema la ibada wakiwa wamebeba vyetezo vyenye moto ndani yake. Dathani na Abiramu, viongozi, wakasimama kwenye hema zao. Mara tu Musa alipomaliza kunena, na mbele ya macho ya Israeli wote, tetemeko la ardhi likawameza Kora, Dathani na Abiramu, na wote waliokuwa wamekusanyika pamoja nao. (m. 29-32). Kisha, watu walipokimbia kwa hofu, moto mbaya ukatoka kwa Yahwe na kuwateketeza wale wakuu 250 pamoja na vyetezo vyao. Kutoka kwenye vile vyetezo, mabamba yalitengenezwa kwa ajili ya madhabahu, kama ukumbusho kwamba ni uzao wa Haruni pekee ambao wangeweza kuteuliwa kwa ukuhani na huduma za maskani (mst. 36-40).

Kuna somo dhahiri hapa la kuheshimu mamlaka. Katika zama ambazo vijana ni wakaidi wa wazi na wakaidi wa mamlaka, vijana wa Ndugu Katika Kristo wanapaswa kuwa waangalifu sana, kuwa watiifu kwa wazazi, walimu na wale wote wenye mamlaka. Tunapaswa kuwa na heshima na kuwapa heshima wale walio na nyadhifa za mamlaka na uongozi duniani na katika eklesia (linganisha. 1 Pet. 2:13-17; 1 Tim. 5:17-19; 1 Thes. 5:12-13). Zaidi ya yote, tunapaswa kutoa heshima, na heshima kubwa zaidi kwa Mungu na Mwanawe, Bwana Yesu Kristo, ambaye hivi karibuni atarudi kuwapa thawabu waaminifu na kuwaangamiza waasi.

UASI ZAIDI.

Hata matukio haya ya ajabu na ya kutisha hayakuwashawishi Israeli. Watu walimlaumu Musa kwa msiba huo, labda wakimhurumia Kora. Walipokusanyika kwa hasira mbele ya hema la kukutania wakiwa na malalamiko yao dhidi ya kiongozi aliyeteuliwa na Mungu, walipigwa na Mungu kwa tauni, na watu 14,700 wakafa. Pigo la kutisha lilisimamishwa tu na maombi ya Musa na Haruni (Mst. 46-47).

 

FIMBO YA HARUNI ILIYOOTA MAUA (Hesabu 17).

Ili kukomesha manung’uniko yote na kuwaonyesha Waisraeli wote waziwazi kwamba alikuwa amemchagua Haruni kuwa Kuhani Mkuu, Mungu aliagiza kwamba, kila kabila lilipaswa kuchagua fimbo, na kuandika juu ya kila fimbo jina la kiongozi wa kabila.. Hayo yaliwekwa mbele ya hema ya kukutania, na siku iliyofuata ilionekana kwamba fimbo ya Haruni ilikuwa imechipua, na si hivyo tu, pia ilikuwa imetoa maua na kutoa lozi. (m.. 8). Hili lilionyesha kwa hakika kwamba aliteuliwa na Yahwe, na mamlaka ya kimungu yaliwekwa ndani yake.

Matukio ya Hesabu 16 yalikuwa yameonyesha kuwa Haruni alikuwa MKUU WA LAWI.

Matukio ya Hesabu 17 yalionyesha kwamba alikuwa KUHANI MKUU KATIKA ISRAELI.

Ilikuwa ni ishara “dhidi ya waasi” kuacha “manung'uniko yote” dhidi ya mamlaka ya Haruni (m. 10).

Ilifundisha watu kwamba wangekufa ikiwa wangethubutu kumkaribia Mungu isipokuwa kupitia Kuhani Mkuu Aliyemteua (ms. 12).

UFUFUO.

Alama ya kuteuliwa kwa Haruni ilikuwa kuchipua kwa fimbo kavu, ambayo ni mfano wa Ufufuo.. Hivyo, katika hili, mfano mzuri wa Kristo ambaye uteuzi wake wa kiungu ulionyeshwa pasipo shaka yoyote kwa kufufuka kwake (Warumi 1:3-4; 1 Wakorintho 15:4-6).. Ukweli kwamba Kristo alifufuka kutoka kwa wafu unaonyesha kuwaMungu amemteua kuwa kiongozi wetu, na si mwingine. Ni lazima tumsikilize, tumfuate, tumtafute Mungu kupitia Yeye - vinginevyo sisi pia tutakufa. Kama vile fimbo ya Haruni “ilivyochanua na kutoa mlozi” vivyo hivyo, ufufuo wa Kristo unatuhakikishia kwamba wengine watazaa matunda (1 Wakorintho 15:14-23).

SOMO KWETU:

Matukio haya ya ajabu yalionyesha kwamba, cheo cha Kuhani Mkuu kilikuwa cha kuteuliwa na Mungu na hakikupaswa kuamuliwa na sauti ya watu. Walijaribu kuweka waliyemtaka, lakini Mungu hakuwapa chochote.

Mungu alimchagua Yesu, na kumteua kwenye nafasi yake, na kwa uwezo wa ujumbe wa injili, anatuchagua sisi. Ikiwa tutasikia sauti yake na kusikiliza ujumbe huo, tunaweza kuwa wafalme na makuhani pamoja na Bwana Yesu katika Ufalme atakaousimamisha (Ufunuo 5:9-10). Watawala wa Ufalme huo hawatawekwa kwa sauti ya watu kwa kura nyingi, bali kwa uteuzi wa kimungu wa Mungu.

MAKTABA YA MAREJEO:

"Mkono wa Mungu Uonekanao" (R. Roberts) Sura ya 18

"Hadithi ya Biblia" (H. P. Mansfield)Toleo la. 2, Kurasa. 81-93

"Musa Mtumishi Wangu" (H. Tennant) Kurasa. 125-141

MASWALI YA AYA:

1.     Eleza uasi wa Kora, Dathani na Abiramu katika Israeli.

2.     Matokeo ya uasi wa Kora, Dathani na Abiramu ni yepi?

3.     Tunajifunza nini kutokana na uasi wa Kora, Dathani na Abiramu?

4.     Je, Mungu aliwathibitishia vipi Waisraeli kwamba alikuwa amemchagua Haruni kuwa Kuhani Mkuu badala ya mkuu mwingine yeyote kati ya makabila mengine 11?

5.     Kuchipua kwa fimbo ya Haruni kunatukumbusha nini (toa sababu zako).

MASWALI YA INSHA:

1. Eleza usuli, changamoto na matokeo ya uasi wa Kora, Dathani na Abiramu.

2. Eleza kusudi na matokeo ya Mungu kutumia fimbo ya Haruni kuonyesha ni nani aliyekuwa Kuhani Mkuu aliyewekwa rasmi na Mungu. Ni kwa njia gani ishara hii inaelekeza kwa Kristo?

 

 

Swahili Title
153. UASI KATIKA ISRAEL
African text
CSSA
Translator 1
Carl Hinton
Translator 2
Jacob Haule
Literature type
Sub type
Sub sub type