Somo la 7
KURUDI KWA BWANA YESU DUNIANI
SOMO: Matendo 1
Miaka 2000 iliyopita
Bwana Yesu alisulubiwa miaka elfu mbili iliyopita. Wafuasi wake walivunjika moyo na kuchanganyikiwa. Matumaini yao yote kwake yalivunjika, alivyokuwa amekufa na kulazwa kaburini.
|
Siku ya tatu, Yesu alitoka kwenye kaburi lile akiwa hai! |
Lakini:
Lilipotokea hili, wafuasi wake waliyakumbuka maneno aliyokuwa amewaambia kabla ya kufa:
âNinyi mtalia na kuomboleza, bali ulimwengu utafurahiâ¦.lakini huzuni yenu itageuka kuwa furahaâ (Yohana 16:20).
Watakuwa walifurahi kiasi gani kumwona Bwana wao mpendwa tena! Tunaambiwa: âBasi wale wanafunzi wakafurahi walipomwona Bwanaâ (Yoh. 20:20). Kwa hakika, furaha yao ilikuwa kubwa sana.
Yesu alipokwenda mbinguni
Sasa hebu soma tena mistari nane ya kwanza ya Matendo 1. Jaribu kupata picha jinsi mitume walivyokuwa katika hizo siku arobaini, Yesu alipokuwa yupo nao tena kwa mara nyingine. Wafikirie tena mwishoni mwa siku hizo arobaini, wakiwa wamesimama juu katika miteremko ya kijani ya Mlima wa Mizeituni, wakiwa na Yesu katikati yao. Ghafla anatwaliwa pale walipo na kupaa mbinguni.
Watakuwa walimtazama sana kwa jinsi alivyoondoka duniani, na kutokomea mawinguni, wasimwone tena. Walikuwa wameachwa ukiwa tena.
Hata hivyo, safari hii hawakufadhaika wala kujiuliza. Hapana! Luka anatuambia tu: ââ¦.. alijitenga nao, akachukuliwa juu mbinguni. Wakamwabudu, kisha wakarudi Yerusalemu wenye furaha kuuâ (Luka 24:51,52).
Siri ya furaha yao
Ni kwa nini baada ya kutengana nao mara hii ya pili walikuwa na furaha kubwa?
Sababu moja ni kwamba, Yesu alikuwa amewaahidi kitu. Alikuwa amewaambia: âTazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahariâ (Mathayo 28:20). Hili lilikuwa na maana kuwa, ingawa walikuwa hawawezi tena kumwona, yeye alikuwa pamoja nao na angeendelea kuwajali siku zote.
Lakini, hiyo haikuwa sababu pekee ya furaha yao. Walipokuwa wakimwangalia akipaa kwenda mbinguni, kuna malaika wawili waliowajea na ujumbe na kuwaambia:
âEnyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi hiyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguniâ (Matendo 1:11).
Wanafunzi wale wote walipokuwa wakirudi Yerusalemu kwa kutii maagizo ya Bwana wao, walikuwa na uhakika kabisa ya kuwa, Yesu mwenyewe angerudi duniani. Hiki kilikuwa ni kitu cha kuwafariji na kuwatia furaha.
Maneno ya Yesu
Yote haya yalitokea miaka 2000 iliyopita, na Yesu bado hajarudi. Lakini tunajua atarudi kwa kuwa ndivyo alivyosema. Katika Luka 21:27 anaongelea kurudi kwake mawinguni, akiwa na ânguvu na utukufu mwingiâ. Utakuwa umegundua kuwa, alipokuwa akipaa aliinuliwa, na âwingu likampokeaâ (Matendo 1:9), na kwamba malaika walisema atarudi, ââ¦jinsi hiyo hiyoâ walivyomwona akienda zakeâ (ms.11).
Mifano mingi aliyotoa Bwana Yesu iliongelea pia kurudi kwake. Chukua kwa mfano, mfano katika Mathayo 25:1-13. Huu unamsemea âbwana-harusiâ, na hatuna tatizo katika kuuelewa. Bwana harusi huyo, hakuna shaka, ni Bwana Yesu Kristo, na simulizi hilo linatutahadharisha kuwa, atakapokuwa akirudi, watakuwepo watu watakaokuwa hawajajiandaa kumpokea. Kwenye mstari wa 13 tutambue kuwa hasemi, âhamjui kama Bwana wenu atarudi au laâ. Hakuna mashaka juu ya hili, ujio wake ni kitu cha uhakika. Analosema ni: âHamwijui siku wala saaâ.
Ushuhuda wa Petro
Siku chache baada ya Yesu kupaa mbinguni, tunasoma juu ya Petro akiwa hekaluni, Yerusalemu, akiwahutubia kwa kishindo Wayahudi waliohusika katika kumsulubisha Yesu. Katika Matendo 3:19,20 anawaambia:
âTubuni basi mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakazi za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana; apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamaniâ.
Petro alisemea tena ujio wa mara ya pili wa Kristo, katika barua aliyoandika baadaye kwa waumini. Akiwasemea wale wasioamini katika 2 Petro 3:4 anasema kuwa, watahoji wakisema: âIko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali hiyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwaâ.
Unaweza ukawa umewasikia watu wakitumia maneno kama hayo. Lakini ni Mungu mwenyewe aliyeahidi kumtuma Bwana Yesu, na tunajua ya kuwa ataitimiza ahadi yake. Petro anaendelea katika mstari wa 9 na wa 10 kusema:
|
âBwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu yeyote apotee, bali wote wafikilie (âwaifikieâ) toba. Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwiviâ. |
Ushuhuda wa Paulo
Yesu mwenyewe alimtokea mtume Paulo na kumtuma aende kuwahubiri wengine. Paulo anadai kuwa Injili aliyokuwa akiihubiri alipewa na Yesu Kristo. Paulo alifundisha juu ya ujio wa mara ya pili wa Bwana Yesu Kristo. Katika 2 Timotheo 4:1 tunasoma Paulo akimwambia Timotheo:
âNakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa kwa kufunuliwa kwakeâ¦â¦.â
Aliandika pia barua mbili kwa kanisa katika Thesalonike. Utaziona nyaraka hizi ndani ya Biblia yako. Ndani yake kuna vifungu vinane vifupi-vifupi, na kuna kitu cha kushangaza ndani yake; katika kila kifungu, Paulo anataja ujio wa Yesu.
Katika 1 Wathesalonike 4:16, anaongelea ufufuo wa wafu katika ujio wa Yesu:
âKwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu, nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanzaâ.
Katika 2 Wathesalonike 1:7,8 Paulo anazungumzia:
âKufunuliwa kwake Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake, katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana Yesu Kristoâ.
Hapa anamwongelea Yesu akirudi kuwaadhibu watu, lakini kama tukiendelea kusoma tutaona kuwa, anawaongelea pia watu wengine ambao, ujio wake utakuwa tukio kubwa la shangwe kwao, kwa kuwa atakuwa anakuja, âKustaajabiwa katika wote waliosadiki katika siku ileâ (ms. 10).
Yesu atafanya nini atakaporudi?
Ujio wa Yesu utayabadili maisha ya kila mtu, atakayekuwa akiishi wakati huo. Litakuwa ni tukio kubwa sana kwa:
- Waumini wanaomsubiri na kumtazamia.
- Wote watakaokuwa wanaishi wakati huo, wasioijua Injili ya kweli.
- Taifa la Wayahudi.
Tuyaangalie haya moja baada ya jingine:
a. Waumini wa kweli wanaomtazamia na kumngoja (Watu walio katika Kristo):
Yesu atawafufua katika wafu wale wote waliokufa katika imani, na kuwakusanya pamoja waumini walio hai:
âAngalieni, nawaambia ninyi siri, hatutalala sote, lakini sote tutabadilika, kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho, maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilikaâ (1 Wakorintho 15:51,52).
Wale ambao wamekuwa si waaminifu watakataliwa, lakini kwa waliokuwa waaminifu, kutakuwa ni shangwe kuu; Yesu atawapa uzima wa milele. Paulo anatuambia katika Wafilipi, Yesu ataubadili: âMwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufuâ (Wafilipi 3:21).
Kama ilivyo kwake, watashirikishwa uzima usio na mwisho; usio na maumivu na machungu yoyote. Watamsaida Yesu katika kazi kubwa ya kuyafundisha mataifa yote juu ya Mungu, na kuwaongoza watu wa dunia waweze kuuitikia upendo wake, na kwenda katika njia zake.
b. Watu wa dunia:
Wakati atakapokuwa akirudi Yesu, hukumu za Mungu zitamwagwa juu ya watenda maovu, na kutakuwa na dhiki kubwa duniani. Hili linasikitisha, lakini haliepukiki. Bila ya Mungu kuitikisa dunia, dunia haitaweza kamwe kumgeukia YEYE na kumkubali Bwana Yesu kuwa Mfalme wake anayemweka.
Baada ya hukumu hizo za Mungu kumwagwa, watu wa dunia watakuwa tayari kumkubali Yesu kuwa Mfalme wao. Naye atausimamisha utawala wa Mungu katika dunia; Ufalme wa Mungu. Uongozi wake utakuwa wa upendo na hekima, wenye kuwajali maskini na wanyonge. Hebu ifungue Zaburi ya 72 na uisome yote. Itakupa picha ya utawala wake. Inasemea vile atakavyowahurumia wenye shida, na wale wasio na msaada.
Watu wa dunia watakaopona katika hukumu hizo za Mungu, wataishi katika Ufalme wa Mungu na kupata mibaraka mingi. Watakuwa, hata hivyo, wakivutwa bado na dhambi, na hatimaye watakufa kama inavyowatokea watu leo. Hata hivyo maisha yao yatakuwa marefu zaidi, na wakati wakiishi watakuwa wakifundishwa Njia za Mungu. Fursa itakuwapo bado kwao ya kuipokea miongozo ya Bwana Yesu, au kuikataa.
Itakapofikia mwisho wa kipindi cha miaka 1000 cha utawala wa Yesu, kutakuwa na ufufuo wa pili na hukumu kwa wale walioishi katika dunia katika kipindi hicho cha miaka elfu moja. Wengi wao watapewa uzima wa milele, na wengine watakataliwa milele. Hatimaye, mauti yatakuwa yametokomezwa; hakutakuwa tena na kufa.
c. Itakuwaje juu ya Wayahudi?
Yesu atarudi katika wakati ambao Taifa la Israeli wapo kwenye hekaheka kubwa. Watakuwa wamezungukwa na maadui pande zote. Yesu, kwa uweza wa Kimungu, atawashinda hao wanaopigana nalo. Ndipo Wayahudi walio wengi watakapotambua hatimaye ya kuwa, Yesu alikuwa ndiye Mfalme na Mwokozi wao kweli waliyeahidiwa, na ambaye walimsulubisha! Nabii Zekaria anasema: âWatamtazama yeye ambaye walimchoma, nao watamwombolezeaâ (Zekaria 12:10). Ndipo sasa watakapomkubali kwa furaha awe Mfalme wao.
Bwana Yesu atausimamisha Ufalme wa Mungu, na Wayahudi watakuwa wakati huo âTaifa Kiongoziâ juu ya mataifa yote. Mji wao Mkuu, Yerusalemu, utakuwa âMakao Makuuâ ya dunia, na kuwa âkitovuâ cha Ibada ya Kweli kwa watu wote. Utakuwa ni wakati wa furaha sana kwa Wayahudi, baada ya mateso yao yote ya miaka mingi. Upendo, furaha na amani ya hali ya juu vitatiririka kwa dunia kutoka katika Makao hayo Makuu mapya!
Kitatokea nini kwako wewe na mimi?
Usome tena mfano ule wa wanawali kumi katika Mathayo 25:1-13. Kama tuna akili nzuri kama wale wanawali wenye busara katika kielelezo hicho, tutajifunza Neno la Mungu, na kujiandaa sasa kwa ujio wa Yesu. Bwana Yesu alipomwambia mtume Yohana, âNaam, Naja upesiâ (Ufunuo 22:20), Yohana alimjibu, âNa uje, Bwana Yesuâ.
Tujiulize, tutakuwa kama mtume huyu na kulifanya jambo hili la kurudi kwa Bwana Yesu liwe jambo la kuombea?
|
Muhtasari
|
Vifungu vya kusoma: 1 Wathesalonike 4, Danieli 12:1-4, Mathayo 25:1-13
Jifunze kwa moyo: Matendo 1: 11
âMalaika wakasema: âEnyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi hiyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguniâ.