SOMO LA 23
SOMO: Mhubiri 3
Baada ya kifo â nini?
Kuna nadharia nyingi zinazotofautiana juu ya nini kinatokea tunapokufa. Ni watu wachache wanaopenda kufikiri wanapokufa inakuwa ndio mwisho wao. Hapa kuna baadhi ya nadharia walizonazo:
- Wapo wanaofikiri wanageuka na kuwa wanyama (huu unaitwa âumwilishoâ).
- Wapo wanaofikiri kuna kitu ndani yao kinachoendelea kuishi mahali fulani.
- Wapo wanaofikiri hakuna tumaini kabisa la namna yoyote ya uhai baada ya kifo.
- Na wengine wanaamini kutakuwa na siku ya ufufuo wa wafu, ikifuatiwa na hukumu, na uzima wa milele kwa waaminifu.
Biblia inasemaje?
Kama tulivyokwishaona, kifo ni adhabu hutokana na dhambi. Kuwa katika hali ya kufa ni kuwa katika hali ya kutotambua chochote; kutokuwa na mawazo ya namna yoyote. Kwa hiyo, mauti ni mwisho kabisa wa uzima na hakuna kinachoendelea kuishi. Andiko linasema:
âWaliohai wanajua ya kwamba watakufa, lakini wafu hawajui neno lolote, wala hawana ijara tena, maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao imepotea yote pamoja, wala hawana sehemu tena katika jambo lolote lililofanyika chini ya juaâ (Mhubiri 9:5,6).
Je, hili lina maana kuwa hakuna tumaini lolote juu yetu? Hakuna tumaini mbele ya kaburi?
Ahadi ya ufufuo na uzima wa milele.
Kusingekuwa na tumaini lolote kama Mungu asingemtuma Yesu Kristo. Yesu mwenyewe alisema: âMsiposadiki ya kwamba mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenuâ (Yohana 8:24).
Lakini kwa sababu ya kile Yesu alichofanya katika maisha yake yasiyo na dhambi na kwa kufa kwake, tunaweza kuwa na tumaini la uzima baada ya kufa. Neno linasema:
âKwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeyeâ (Yohana 3:16,17).
Tunaweza kusamehewa dhambi zetu kupitia kwa Yesu. Yesu alisemewa na Yohana Mbatizaji kuwa ni: âMwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwenguâ (Yohana 1:29). Tunakufa kwa sababu ya dhambi. Kama dhambi zetu zinasamehewa kabisa, hatuwezi kubakia tumekufa. Tunakuwa kama ilivyokuwa kwa Yesu.
Jisomee mwenyewe Yohana 6:39,40,44. Tunajua ya kwamba Yesu anaongelea hapa kufufuliwa kwa wafu mara tatu, âsiku ya mwishoâ. Hasa katika msitari wa 40 anasema: âMapenzi yake baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele, nami nitamfufua siku ya mwishoâ.
Ufufuo wa wafu unaongelewa pia katika Yohana 5:28,29. Yesu anasema:
âMsistaajabie maneno hayo, kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka, wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumuâ.
Nabii Danieli naye alilisemea hili akionesha kuwa, ni sehemu tu ya wale watakaofufuliwa watakaopewa uzima wa milele: âTena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa mileleâ (Danieli 12:2).
Kwa hiyo, kutakuwa na hukumu. Tunaambiwa kuwa, wale watakaokuwa hai wakati wa kurudi Yesu, watahusika pia na hiyo hukumu. Yesu atawahukumu: âWalio hai na waliokufa, kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wakeâ (2 Tim 4:1).
Hao watu watakaoonekana wanafaa, watapewa nafasi katika Ufalme wa Mungu utakaoanzishwa hapa duniani. Yesu atawaambia:
âNjoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwenguâ (Mathayo 25:34).
Hawa watu waliokuwa waaminifu watapewa uzima wa milele; maisha yaliyo makamilifu na yasiyo ya dhambi. Tunasoma katika Luka 20:35,36 kuwa, watakuwa kama malaika:
âWale wahesabiwao kuwa wamestahili kuupata ulimwengu ule, na kule kufufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, wala hawawezi kufa tena, kwa sababu huwa sawasawa na malaika, nao ni wana wa Mungu, kama vile walivyo wana wa ufufuoâ.
|
Tumaini la Mkristo lipo katika ufufuo wa kimwili kutoka kwa wafu, na nafasi katika Ufalme wa Mungu katika dunia hii atakaporudi Yesu. |
Wadhambi wanakwenda motoni?
Je, kuna hasa sehemu ya kutisha inayoitwa âkuzimuâ watu waovu wanapokwenda kuteswa baada ya kufa? Tumeshaona kuwa, mtu anapokufa, uhai wake unakuwa umefikia mwisho moja kwa moja! Hawezi tena kufikiri au kuhisi chochote. Kwa hiyo âkuzimuâ ni nini, na ni wapi?
Neno âkuzimuâ ni neno lenye maana ya âmahali palipofichwaâ au âmahali palipofunikwaâ. Ni neno linalotumika katika Biblia kumaanisha mahali palipofichika au palipofunikwa kwa ajili ya wafu; ni kaburi.
|
Maana ya âkuzimuâ ni âKABURIâ |
Katika Agano la Kale, neno la Kiebrania lililotafsiriwa âkuzimuâ ni âsheolâ. Limetumika katika vifungu vifuatavyo:
|
Katika Zaburi 49:15 mwandika Zaburi anasema: âMungu atanikomboa nafsi yangu, atanitoa mkononi mwa kuzimuâ. |
|
Katika Zaburi 55:15 mwandika Zaburi anasema: âMauti na iwapate kwa ghafla, na washuke kuzimu wangali haiâ. |
Neno hili âkuzimuâ ni neno âsheolâ; halina maana nyingine. Sio mahali pa ajabu-ajabu, pasipoeleweka.
Katika Agano Jipya, neno lililotafsiriwa âkuzimuâ ni âhadesâ katika Kiyunani.
|
Katika Ufunuo 1:18 Yesu anasema: ââ¦â¦..Ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimuâ. |
|
Katika 1 Wakorintho 15:55, mtume Paulo anasema: âKu wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?â |
Neno âmautiâ na neno âkuzimuâ, yote ni neno âhadesâ katika lugha ya Kiyunani; maana yake ni moja (Kiyunani ndiyo lugha ya asili iliyotumika kuandika Agano Jipya lote; lugha zingine zote ni tafsiri).
Hili linatuonesha kuwa, katika Agano la Kale na Agano Jipya, neno âkuzimuâ lingeweza kutafsiriwa âkaburiâ moja kwa moja.
|
Maana ya kuzimu ni âKABURIâ |
Kwa hiyo, kuzimu sio mahali pa kutisha pa mateso kwa ajili ya wadhambi wanapokuwa wamekufa.
Yesu alirudi kutoka kuzimu
Baada ya Yesu kufufuka kutoka kwa wafu na kupaa mbinguni, Petro aliwahubiri watu waliokusanyika Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu ya Pentekoste. Aliwaambia kuwa, mfalme Daudi alikuwa amemtabiria Yesu kufufuliwa kutoka kwa wafu. Unabii huu unapatikana kwenye Zaburi ya 16, na Petro anauongelea katika Matendo 2:27 akisema:
âKwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu, wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifuâ.
Petro anasema kuwa, Daudi alikuwa akimtabiria Yesu Kristo:
âYeye mwenyewe (Daudi) akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifuâ (ms.31).
Roho yake Kristo (yaani, Kristo mwenyewe) hakuachwa kuzimu (yaani, kaburini) kwa kuwa Mungu alimfufua siku ya tatu. Mtakatifu wa Mungu hakuona uharibifu (yaani, hakuishia mautini).
Katika Ufunuo 1 Yesu anazungumzia ufufuo wake mwenyewe, na pia ahadi yake ya kuwafufua wafuasi wake waaminifu, anaposema:
âNalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimuâ (Ufun. 1:18).
Wafuasi wa Yesu waliokwisha kufa, wamefungiwa katika makaburi (au kuzimu). Yesu anao ufunguo (anao âuwezaâ) wa kuyafungua makaburi hayo wakati akirudi, na kuwafufua waliokufa na kulazwa humo.
Kuzimu (âhadesâ)
Mara nyingine âkuzimuâ kunafikiriwa kuwa ni mahali pa giza au ukungu mnene zinapokaa roho za watu waliokufa. Tunajua hili haliwezi kuwa kweli kwa kuwa Biblia inatuambia: âWafu hawajui neno loloteâ (Mhubiri 9:5).
Hakuna mtu aliyekufa anayejua kitu; anayepata raha au maumivu, kwa kuwa hakuna wanachotambua. âKuzimuâ tumeshaona, ni âkaburiâ tu.
Vipi juu ya moto wa kuzimu; wa milele?
Yesu anasema mara tatu katika Marko 9 juu ya âmoto usiozimikaâ. Anasema:
âNi afadhali kuingia katika uzima u kigutu, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako Jehanum, kwenye moto usiozimikaâ (Marko 9:43).
Sasa Yesu hapa alimaanisha nini?
Neno âJehanumâ katika msitari huo ni neno âGehennaâ katika Kiyunani, linalotokana na neno âGhi-Hinnomâ katika Kiebrania. Ghi-Hinnom lilikuwa ni jina la bonde lililokuwa nje kidogo ya jiji la Yerusalemu. Ni mahali ambapo miaka ya nyuma wafalme wa Israeli waliteketezea watoto wao kwa moto, wakitambikia miungu ya kigeni (unaweza kusoma juu ya hili katika 2 Wafalme 23:10).
Katika kipindi cha Yesu, hilo âBonde la Hinnomâ (Jehanum) lilikuwa ni mahali mizoga ya wanyama na takataka za Yerusalemu zilipoteketezewa. Moto ulikuwa ukiwaka hapo wakati wote; lilikuwa ni âdampoâ la jiji. Palikuwa mahali pa kitu kuteketezwa kitu moja kwa moja.
Yesu alipolitumia neno âJehanumâ walielewa alikuwa akisemea mahali hapo, ikiwa ni ishara ya kuharibiwa au kuteketezwa moja kwa moja; kuangamia. Hakuwa akisema watu kuteseka kwenye adhabu isiyo na mwisho ya moto. Mungu wa upendo hawezi kufanya hivyo. Wangeangamia kwa kufa.
|
Muhtasari
|
Kifungu cha kusoma: Yohana 11:1 â 45
Msitari wa kujifunza: 1 Wakorintho 15: 22,23:
âKwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika katika Kristo wote watahuishwa. Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo, baadaye walio wake Kristo, atakapokujaâ.