Somo la 29
IBILISI, MAPEPO, SHETANI
Somo: Mathayo 8:14-34
IBILISI NA PEPO
Kuna maneno mawili ya Kiyunani yaliyotafsiriwa âIbilisiâ katika Biblia zetu, na kwa kuwa yanamaanisha vitu tofauti, tutahitaji hasa kujua kila neno lina maana gani. Maneno hayo ni:
Daimon â lenye maana ya âroho mbaya au roho mwovuâ
Diabolos â lenye maana ya âmsingiziaji au mchongeziâ
Tutalichunguza neno Ibilisi (diabolos) katika somo litakalofuata. Neno âdaimonâ linatumiwa katika Kiyunani tunapoambiwa, Yesu: âakawatoa pepoâ. Yesu aliponya magonjwa yote watu waliyokuwa wakiugua. Aliwapa vipofu kuona, aliwezesha viziwi kusikia, aliwafanya na walemavu wa miguu kutembea. Yesu aliwaponya pia watu wengi waliokuwa na magonjwa ya kiakili; kichaa na matatizo kama ya kifafa.
Katika siku hizo, kama ugonjwa ulikuwa mgumu kueleweka, watu walisema kuwa mgonjwa huyo alikuwa, âameshikwa na pepoâ. Soma kwa makini Mathayo 8:16,17. Tunaambiwa hapa kwamba:
|
ââ¦wakamletea (Yesu) wengi wenye pepo; akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote waliokuwa hawaweziâ. |
Yesu akawaambia, Isaya alikuwa ametabiria jambo hilo, aliposema:
|
âMwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, na kuyachukua magonjwa yetuâ (Isaya 53:4). |
Hili linatufundisha kuwa:
|
âKushikwa au kukamatwa na pepoâ ni sawa na âUdhaifu na magonjwaâ. Yesu aliwaondolea madhaifu na magonjwa hayo. |
Sanamu (miungu ya wongo) iliyokuwa âpepoâ
Katika sehemu zingine kwenye Biblia ambapo neno âdaimonâ lilitumika, mara nyingi lilikuwa likiongelea ibada za miungu ya uwongo. Tuangalie Zaburi ya 106.
Zaburi hii inatuambia juu ya makosa mengi Waisraeli waliyokuwa wakiyafanya na vile, pamoja na hayo, Mungu alivyoendelea kuwabariki. Soma msitari wa 36-38 mwandika-Zaburi anaposema juu ya wana wa Israeli kuwa:
âWakazitumikia sanamu zao, nazo zikawa mtego kwao. Naam, walitoa wana wao na binti zao kuwa dhabihu kwa mashetaniâ.
Neno âmashetaniâ, hapa ni neno âdaimonâ katika Kiyunani, lililotafsiriwa pia âpepoâ, kwenye Kiswahili. Katika msitari wa 37 shutuma dhidi yao zimerudiwa, lakini hapa tunaambiwa kuwa: âWaliwatoa wana wao na binti zao kuwa dhabihu kwa mashetaniâ. Ni wazi basi kuwa, âmashetaniâ wanaotajwa hapa, walikuwa ni sanamu; miungu ya uwongo ya mataifa yaliyokuwa yakiizunguka Israeli.
Kuna matumizi ya neno hili katika Agano Jipya yanayoleta maana hiyo hiyo katika 1 Wakorintho 10:20. Mtume Paulo anawaambia Wakorintho ya kwamba, vitu vile watu wa kimataifa: âWavitaovyo sadaka, wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Munguâ.
Kama ukirudi nyuma kwenye msitari wa 19 utaona kuwa, hayo âmashetaniâ yalikuwa, âsioâ kitu. Yalikuwa sanamu; miungu isiyokuwa ya kweli ya watu wa kimataifa, wasiomjua Mungu.
Wakristo wamepewa kumwabudu Mungu mmoja tu aliye wa kweli, miungu mingine yote ni sanamu, hapa ikiitwa âmashetaniâ. Vitu visivyo na uhai watu wanaviabudu bure; ni ukafiri.
Angalizo: Neno lenye maana ya âroho mbaya au roho mwovuâ (daimon) kwa kawaida limetafsiriwa âpepoâ, lakini lisichanganywe na neno âIbilisiâ. Sehemu zingine, neno, âmashetaniâ limetumika badala ya pepo.
SHETANI
Neno âshetaniâ katika Agano la Kale lina maana ya âaduiâ au âanayepingaâ. Mfano wa jinsi lilivyotumika upo katika 1 Wafalme 11:14 ambapo tunasoma, kuwa: âNdipo BWANA akamwondokeshea Sulemani adui, Hadadi Mwedomiâ. Na mbele kidogo kwenye 1 Wafalme 11:23-25 tunaambiwa: âTena, Mungu akamwondokeshea adui mwingine, Rezoni mwana wa Eliadaâ¦Naye akawa adui wa Israeli siku zote za Sulemaniâ.
Sulemani alianza ufalme wake vizuri akimpenda sana Mungu, lakini baadaye alinasa katika kuabudu sanamu. Matokeo yake, Mungu alimwondokeshea maadui ili asipate amani. Neno hilo âaduiâ ni neno hilo hilo lililotafsiriwa âshetaniâ sehemu zingine.
Hadadi na Rezoni walimsumbua Sulemani na Israeli (âwaliwapingaâ) na sababu ni kuwa, Sulemani na Israeli walikuwa wamemkiuka Mungu; walikuwa wakifanya dhambi. Hadadi na Rezoni walikuwa âshetaniâ kwa Sulemani na Israeli.
Lakini, katika Biblia âshetaniâ sio mara zote anakuwa adui mbaya. Katika Hesabu tunaambiwa juu ya nabii aliyekuwa akiitwa Balaamu, aliyekuwa akienda safari ambayo Mungu hakuwa akitaka aende. Maandiko yanasema:
âHasira ya Mungu ikawaka kwa sababu (Balaamu) alikwenda; malaika wa BWANA akajiweka njiani, ili kumpingaâ (Hes. 22:22).
Neno âkumpingaâ hapa pia ni neno âshetaniâ katika Kiebrania. Hapa âshetaniâ alikuwa ni malaika mwaminifu wa Mungu anayefanya mpenzi ya Mungu, aliyetumwa kumzuia Balaamu njiani asiende kuwalaani wana wa Israeli.
Ni wazi neno hilo haliwezi kumaanisha kiumbe mwovu, au malaika mwovu. Hakuna malaika anayeweza kuwa mwovu. Shetani ni adui, mpinzani; mtu anayepinga. Anaweza kuwa mwema au mbaya.
|
MAANA YA SHETANI NI ADUI AU MPINZANI; MTU ANAYEZUIA |
Wakati Petro alipojaribu kumzuia Yesu asiiendee njia ambayo Mungu alimtaka aiendee; njia ya msalaba, Petro alikuwa âaduiâ. Yesu alimwambia Petro: âNenda nyuma yangu, Shetani, u kikwazo kwanguâ. Sababu ni kwamba, Petro alikuwa akitaka kumgeuza Yesu asiufuate mpango wa Mungu. Yesu anamwambia, âHuyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamuâ (Mathayo 16:23).
Kwa hiyo, Petro alikuwa âshetaniâ; alikuwa hapa akimpinga Yesu; akipingana na kusudi la Mungu. Unaweza kuona; hata katika Agano Jipya maana ni ile ile. Adui mkubwa kuliko wote wa mtu ni hulka yake mwenyewe ya dhambi.
Neno âshetaniâ linaweza kutumiwa kwa hiyo hulka. Hili linaweza kuonekana tena vizuri kwa kulinganisha Matendo 5 msitari wa 3 na wa 4.
|
Ms.3: âPetro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu na kuzuia kwa siri sehemu ya kiwanja?â |
Ms.4: ââ¦ilikuwaje hata ukaliweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu....â |
Ni mawazo yaliyokuwa potofu ya Anania yaliyomfanya afanye vile. Neno âshetaniâ limetumiwa katika mstari wa 3 kuiwakilisha hulka ya dhambi aliyokuwa nayo Anania, iliyokuwa ikiyapinga nafsini mambo ya kiroho; mambo ya Mungu.
Lusifa alikuwa ni nani?
Watu wanaoamini juu ya uwepo wa âduduâ ovu linaloitwa âshetaniâ lisiloonekana, wanapenda kuthibitisha kuamini kwao kwa kunukulu mara nyingi Isaya 14:12-16. Mistari hiyo inasema:
âJinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa uliyewaangusha mataifaâ¦.â
Maneno, ânyota ya alfajiriâ katika Biblia ya Kingereza ni âLuciferâ (Lusifa). Kwa hakika, kama ukikisoma kifungu hicho chote (Isaya 14), utaona kuwa, Lusifa ni mfalme wa Babeli, âmwenye kuoneaâ (anayeelezewa kwenye mstari wa 4). Ulikuwa ni unabii wa kuanguka kwa ufalme wa Babeli; kitu kilichotokea miaka ilivyopita.
Kwa namna hiyo hiyo, Ezekieli 28:14-16 mara nyingine inasemewa kusemea uwepo wa âduduâ hilo:
âWewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Munguâ¦.Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yakoâ.
Ni wazi kuwa ujumbe huu ulikuwa ni kwa ajili ya mfalme wa Tiro, kama mstari wa 12 unavyosema, na hauhusiani na uwepo wa âduduâ lolote hai ovu lisiloonekana.
Ni nini kilichotokea katika Bustani ya Edeni?
Unakumbuka ni nini kilichotokea katika Bustani ya Edeni? Mungu alipomwita Adamu kutoka mahali alipojificha na kumuuliza kama alikuwa amekula kutoka katika mti wa ujuzi wa mema na mabaya, Adamu alijibu: âHuyo mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda ya mti huo, nikalaâ (Mwanzo 3:12).
Ukilitafakari jibu hilo utaona kwamba, Adamu alikuwa ni kama anamwambia Mungu kosa sio lake; ni la Mungu. Yeye ndiye aliyempa huyo mwanamke, na mwanamke ndiye wa kulaumiwa kwa kumpa hilo tunda. Lakini, kosa lilikuwa ni la kwake mwenyewe.
Kisha Mungu akamuuliza mwanamke alichofanya ni nini, na mwanamke akajibu: âNyoka alinidanganya, nikalaâ. Kwa maneno mengine, alimtupia lawama nyoka; lilikuwa ni kosa la nyoka.
Adamu na Hawa walikuwa na shauku ya kutupia lawama kwingine, badala ya kubeba lawama wenyewe kwa makosa yao. Sisi wote tumekuwa hivyo. Hatupendi kuwajibishwa kwa mawazo na matendo yetu mabaya wenyewe; hatupendi kukubali kosa. Pengine ndio maana watu wengi wanapenda kuamini kuwa, kuna âduduâ hilo lisiloonekana linaloitwa âshetaniâ linalowadanganya watu wamwasi Mungu.
Mungu alimruhusu nyoka kuongea; sio ajabu sana. Ni kama alivyomruhusu punda wa Balaamu kuongea katika Hesabu 22:28.
Adamu alipaswa kujidhibiti na kumkataa nyoka, lakini Mungu aliwaacha Adamu na Hawa wajaribiwe, na wakaanguka. Nyoka hakuwafanya walile lile tunda; alichofanya tu ilikuwa kuwajaribu. Adamu na Hawa hawakumtii Mungu; walijiamulia wenyewe kufanya walichotaka.
Muhtasari
|
Vifungu vya kusoma: Mathayo 16:21-28, Hesabu 22
Mistari ya kushika: Mathayo 8:16, 17
âHata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo; akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote waliokuwa hawawezi, ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, na kuyachukua magonjwa yetuâ.