313. YONA MTUME
"Wokovu ni wa Bwana"
Kufuatia utawala wa Yehu, mfalme wa Israeli, kiti cha enzi kilichukuliwa na Yehoahazi, Yohoshi (inayojulikana pia kama Yoashi) na kisha Yeroboamu II Wakati wa utawala wa Yeroboamu II manabii Yona, Hosea, Isaya, na Amos walitabiria taifa. Yona alitambua kwamba mafanikio ya taifa la Israeli kwa wakati nguvu za Washuri zilikuwa zikishuka. Hata kama Israeli ilikuwa ina mafanikio kisiasa na kiuchumi, Yona alikuwa anajaribu kuzuia uozo wa kiroho.
Wakati alipewa maagizo na Yawheh kuhubiri toba kwa Washuri, Jona aliona matokeo yasioepukika- - kwamba wangetumika kuleta adhabu kwa Waisraeli, watu wake wapendwa. Akipewa motisha na kile kilicho-onekana kama nia nzuri; alitaka kuepuka amri ya Mungu.
Lengo la somo hili ni kuona kwamba kuona kwamba hakuna mtu anayeweza kuzuia kusudi la Mungu na uchaguzi wake; wale wanaotubu watapokea huruma, lakini waasi wataharibiwa
Yona
YONA, MTU (Yona 1:1).
Yona mwenyewe alikuwa wa Gath-heferi, kijiji kidogo katika Galilaya kilomita tano kaskazini-mashariki mwa Nazareti. Alikuwa mwana wa Amitai (kutoka "Emeth" maana yake "ukweli"). Jina lake, maana yake âNjiwaâ kuashiria alikuwa âNjiwa wa Kweliâ. Alikuwa yule aliyeonyesha kujali kwa maslahi ya ndungu zake, tabia inayofaa kwa wanaomfuata Mungu. Katika hili,akawa na bidii zaidi ya kuondoa hukumu ya kweli ya Mungu kutoka kwao.
YONA ANAJARIBU KULETA MAGEUZI YA KITAIFA (2 Wafalme 14:23-29)
Matukio ya kitabu cha Yona yalitokea wakati wa utawala wa Yeroboamu II, mfalme wa Israeli (kk 799-759). Historia ya nyakati imewekwa katika kumbukumbu ya 2 Wafalme 14: 23-29. Israeli ilikuwa imepungua kutokana na mateso na Mungu alikuwa tayari kuwapa nafasi ya mwisho, ili wabadilike na wamrudie. Kusudi lake halikupaswa kufutika kabisa (Mai.3;6) hivyo akamwinua YeroboamuII, mwana wa Yoashi, lakini alikataa njia ya Bwana kama ilivyonenwa na Yona, na badala yake akachagua njia ya Yeroboamu I. Mwana wa Nebati (Mst.24) Hata hivyo Israeli aliokolewa kutoka kwa maadui zake "kwa mkono wake" (Mst.26-27), na katika kipindi hiki cha utawala dhabiti ulionawiri na mipaka ikapanuka. Yona alikuwa ametabiri hili (Mst.2) kwa upande wa Kaskazini mpaka ulipanuliwa hadi "kuingia Hamathi", Wakavamia Washami na kuokoa Damasko, kwa upande wa kusini Yeroboamu aliteka nchi kwa umbali wa hadi âBahari ya Arabaâ ikimaanisha ilikuwa hadi Edomu (Mst.25, Kum. 3:17;. 4:49).
UTUME WA YONA (Yona 1:2).
Wakati Israeli ilikuwa katika hali ya kushuka maadili, Yona alipewa kazi ya kuhubiri msamaha kwa watu wa Nineve, mji mkuu wa Ashuru. Alikuwa aonye watu kwamba mji utaangushwa ndani ya siku 40 kama hawatatubu.
YONA ANATOROKA KUTOKA BWANA (Yona 1:3-16).
Yona alitambua kwamba kushuka kwa Ashuru kulitokana na dhambi zao na pia kwamba kama wangetubu, wangeweza kuokolewa na kufanikiwa. Alihofia kwamba wangeweza kutishia usalama wa Israeli. Hata kama israeli walikuwa wamemwacha Mungu, Waashuri walikuwa wenye kiburi na wakaidi. Hakuona sababu ya kuwaokoa watu wa Shamu. Hivyo alijaribu kuepuka amri ya Mungu kwa kutorokea Yopa na kisha kuchukua mashua hadi Tarshishi (Mst.3). Labda alifikiria kwamba kama kutubu kwa Nineve kungecheleweshwa kwa siku 40 basi Nineve ingekuwa imeharibiwa (3;4) Hakuelewa kwamba neema ya Mungu ingeenezwa kwa watu wote na hakuna mtu alikuwa na ruhusa ya kuweka kipimo kwa huruma ya Mungu (linganisha. 20:15 Mt.). Mungu anawapenda wanadamu kutoka kila taifa la Ufalme wake Mwa. 12: 1-3; Mdo. 10:28, 34-35). Ilibidi Yona ajifunze kwamba wanadamu wote watakuja kutubu, hata kama alikuwa amewapa waisraeli upendeleo maalum (1Tim. 2: 4).
Wakati Meli ilipongoa nanga, Yona alienda kulala chini. Lazima iwe alikuwa amechoka kwani alilala wakati kulikuwa na dhoruba kali. Meli ilikuwa hatarini ya kuvunjika (Mst.4) Mabaharia walifanya kazi kwa bidii na kutupa baharini vyombo ili kufunya meli kuwa nyepesi (Mst.15) kila mmoja alimwita mungu wake aje awasaidie. Walipompata Jona amelala, walimwamsha ili pia yeye apate kuomba (Mst.6)
Walishuku kwamba Mmoja wao alikuwa wa kulaumiwa kwa matatizo. Wengi walishukiwa na Yona akasema ndiye chanzo cha matatizo yake (Mst 7) walimuuliza maswali (Mst 8), na akakiri alikuwa mwebrania aliyeabudu "Bwana, Mungu wa mbinguni, ambaye ameumba bahari na nchi kavuâ. Kwa hivyo alitawala kila kitu na alikuwa na uwezo wa kutiliza bahari (Zab. 65: 7; 89: 9; 107: 25-30; Mt. 8:26.). Aliwaambia kwamba alikuwa ametoroka kutoka kwenye uwepo wa Mungu. Wakamuuliza kwa jinsi gani bahari ingetulizwa. (Mst. 9-10), na alipopendekeza wamtupe baharini, walishikwa na hofu. Jona alikuwa ametambua kwamba dhoruba hii ilikuwa imeletwa kwa sababu yake na alikuwa tayari kujiyatoa maisha yake kwa sababu ya wale waliokuwa kwenye meli. Pia angeweza kutoroka kazi aliyoichukia ya kuleta msamaha kupitia toba kwa adui wa Israeli. (4:3) Israeli ingeokolewa kupitia kifo chake.
Walijaribu kudhibiti meli kwa kutumia makasia, lakini juhudi zao zilikuwa za bure (Mst.13). Wakahitimiza kwamba njia pekee ya kujiokoa ilikuwa kupitia kifo cha Yona, lakini hawakuwa wanataka kulaumiwa kwa kifo chake. (Mst.14) Walinganishe na pilato aliyetaka kujiondolea hatia ya damu ya kristo.
Baada ya Yona kutupwa baharini, dhoruba ilitulia (Mst.15) na mabaharia wakaamini nguvu za Mungu. Wakamtolea sadaka na kuapa kumtumikia.
MAISHA YA YONA YANAHIFADHIWA (Yona 1:17; 2)
Yona alitupwa katika bahari chafu. Na akazama ghafla na magugu ya baharini yakamzunguka kichwa chake. Alipozama hadi chini, alifikiria maisha yake yameishia katika kaburi la maji, wakati huo kitu cha ajabu kilitokea. Samaki mkubwa, aliyetayarishwa na Mungu, akammeza; Alibakia tumboni mwa samaki kwa siku tatu, mpaka, kwa amri ya Mungu, samaki akamtapika katika nchi kavu. Yona.2:2-9 ni kumbukumbu ya maombi yake akitoa shukrani baada ya kuokolewa kutokana na kifo. Katika kukata tamaa, "nje ya tumbo la kuzimu" (Ebr. "Sheol" = kaburi), alipiga kelele kwa Mungu na sauti yake ilisikika. Bwana alikuwa amekuwa wokovu wake: âWewe umeleta maisha yangu kutoka kwenye upotofuâ, akasema, kifo hiki, mazishi na ufufuo wa Yona ulikuwa mfano, kwani Yesu aliongea kuhusu âIshara ya nabii Yonaâ akasema âkama vile Yona alikuwa ndani ya tumbo la nyangumi kwa siku tatu mchana na usiku; hivyo ndivyo Mwana wa Mtu atakuwa kwa siku tatu na usiku katika roho ya nchiâ (Mt. 00:40;. Yona 1:17).
YONA ANAHUBIRIA NINEVE (Yona 3)
Juu ya nchi kavu, Yona alikuwa amepewa kazi na Bwana, âInuka, uende Ninawi, mji ule mkubwa, ukahuburi habari nitakayokuamuruâ (Mst. 1-2) Wakati huu alitii na akelekea mji wa Nineve, ambao ulikuwa mkuu na ulichukua siku tatu kuufikia- pengine umbali wa kilomita 100 (Mst. 3) akielekea hadi katikati mwa Nineve alipiga kelele â Baada, siku arobaini Ninawi itangamizwaâ (Mst.4) Aliwasihi waache njia zao potovu na kumtumikia Mungu).
Ujumbe huu ulio wazi ulikuwa ule watu walihitaji. Ujumbe ulikuwa wa nguvu na ulipata majibu ya haraka, ukafikia watu wa kawaida na hata mfalme aliye kwenye kiti cha enzi. Alitoa wito kwa watu watubu kuachana na dhambi na vurugu. (Mst. 6-9) kwa kuona tabia yao ya kutubu, Mungu aligeuza nia yake na kuepusha Ninawi. (Mst.10) Hii ni tabia yake ya kukabiliana na binadamu (Tizama Yer. 18: 6-10). Wakati binadamu yu tayari kuacha njia zake mbaya, Huruma ya Mungu inapatikana. Akikataa huruma yake, hukumu inakuja kwa haraka, kama ilivyokuwa Ninawi wakati wa Nabii Nahumu.
KUKATA TAMAA KWA YONA (Yona. 4:1-3).
Yona alikuwa amefikisha ujumbe wa Mungu Ninawi, lakini alikatishwa tamaa na mafanikio ya mafunzo yake (Mst.1) Moyo wake ulikuwa kweli na Israeli kwani aliwafanyia mageuzi kwa bidii sana. Kutubu kwa Ninawi kulileta huruma ya Mungu, lakini hili lilimfanya akasirike.Alibishana na Mungu,akisema kwamba heri afe kuliko kuona Ninawi ikitubu! Hii ilikuwa sababu iliomfanya kutoroka hapo awali, Alisema (Mst.2) Alihofia kwamba Mungu angebadilisha fikra zake na kukataa kuharibu Ninawi, adui wa Israeli.
Tunaona mageuzi ya ajabu katika akili ya Yona. Hakuweza kutambua kwamba Mungu angekuwa na uhusiano na taifa lingine. Israeli katika macho yake walikuwa na haki ya kipekee ya huruma ya Mungu. Ilimbidi ajifunze kwamba Bwana âAmbaye aliumba bahari na nchi kavuâ (1:9), alikuwa Mungu wa Watu wa Mataifa na pia wa Wayahudi (Rum. 3.29)
YONA ANAPATA FUNZO â MFANO WA MTANGO (Yona 4:4-11)
Bwana alimjibu Yona kwa njia ambayo iliitia nia yake changamoto, âumefanya vizuri kukasirika?â Yona aliondoka mjini, akatengeneza kibanda (makao ya muda kama yale Waisraeli waliyotengeneza wakati wa sherehe ya vibanda (Law. 23: 41-44), na akasubiri kuona hatma ya Ninawi. Mungu alisababisha mmea mkubwa kumea karibu na Yona na kumpa kivuli zaidi, naye alifurahishwa na hili. Lakini usiku mmea huu wa mmbuyu uliliwa na wadudu. Mungu alikuwa kwa njia ya ajabu, anatayarisha matukio ambapo Yona angeelewa makosa ya chuki yake pamoja na ukuu wa Mungu, kama Mungu wa Wayahudi na Watu wa Mataifa. Kesho yake jua lilichomoza na Mungu akasababisha upepo wenye nguvu kutoka Mashariki ukapiga. Yona aliomboleza kupoteza mmea wa Mtango na akatamani kufa. Akimkuta katika hali ya kutotubu, Mungu kwa mara nyingine alimuuliza, â Je umefanya vyema kukasirika kwa ajili ya Mtango?â Yona akafanya moyo kuwa mgumu akajibu; â nimefanya vizuri kukasirika, hata kutamani kufaâ. Maswali ya Mungu yalionyesha alikuwa anastahili kubadilisha jinsi alivyofikiria. Alikuwa amesababisha watu wa Ninawi watubu lakini alishindwa kutubu (linganisha 1Kor. 9:27).
Upumbavu wa msimamo wake unaletwa mbele yake katika taarifa ya Mungu inayohitimisha kitabu hiki âWewe umeuhurumia mtango, ambao huku-ufanyia kazi, wala kuuotesha; uliomea katika usiku mmoja na kuungamia katika usiku moja, na Mimi je! Haikunipasa kuhurumia Ninawi, Mji mkuu, ambapo ndani yake kuna watu zaidi ya mia ya ishirini elfu ambao hawawezi kupambanua kati ya mkono wao wa kulia na wa kushoto; tena wamo wanyama wa kufungwa wengi sana?
Yona alikuwa na huruma kwa mmea, kwa sababu ulimpa kivuli kizuri, kuliko binadamu. Binadamu alikuwa kiumbe wa mwisho kuumbwa na Mungu, Taji la uumbaji aliyeumbwa katika sura na mfano wake. Yona, alikuwa analaani Mungu kwa kuwaokoa binadamu aliyewaumba. Mtungo, ambao Yona hakuwa ameufanyia kazi, kama binadamu, ambaye si kama binadamu, ambayo angesihi kwa siku chache angependelea kuona wameokoloewa. Somo ni dhahiri. Mungu ni mwokozi wa kila binadamu; Hayuko tayari kuachilia yeyote kuangamia, lakini inabidi waje kwake kwanza na KUTUBU, kama Ninawi ilivyofanya na wakaishi (1 Tim.2: 4; 2 Pet. 3: 9; Eze. 18:23, 32).
ISHARA YA NABII YONA (Mathayo 12:38-41)
Wakati Mafarisayo walitaka ushahidi wa kuonyesha kwamba Yesu Mesia wa Israeli alijibu, âkizazi kiovu kisicho na uaminifu wanatafuta ishara; na hakutakuwa na ishara itakayotolewa isipokuwa na nabii Yonaâ. Akaendelea kuelezea njia mbili ambazo Yona alikuwa Ishara.
- Mst.40. Yona kwa siku 3 na usiku 3 akiwa katika tumbo la samaki mkubwa ilikuwa ni ishara kwamba yeye pia, ilikuwa katika moyo wa nchi kwa kipindi hicho.
-
Mst.41. Katika mstari huu anatofautisha mapokezi kwamba watu wa Ninawi walimpa Yona ujumbe kwa njia ambayo yeye alikuwa amepokelewa.
Waninawi walikuwa wametubu, lakini walikuwa "kizazi kiovu kisicho na uaminifu" (Mst.39), na kwa kirefu wangekuja kumsulubisha. Na Wayahudi katika siku za Yesu walikuwa na kila sababu ya kutubu, kwani walikuwa tayari wamepewa ishara nyingi, ambazo zilidhihirisha alikuwa Mesia (Yn. 15:24.). Kwa sababu hizi wangeweza kuhukumiwa na Ninawi katika siku ya hukumu.
Ni jambo la kuvutia kulinganisha Yona na Yesu na Petro.
YESU NA PETRO
Kama njiwa Roho Mtakatifu, chanzo cha Ukweli, alishuka juu ya Yesu (Mt.3:16; Yn.16:13). Petro, au "Simoni mwana wa Yona" (Yn.21:15), alipewa kazi ya kupeleka injili kwa mataifa kutoka Yopa (Mdo.10: 5). Alikuwa ana chuki dhidi ya mataifa (Gal. 2:12). Watu wa Mataifa walitubu (Mdo.10:48). Yesu aliwaonya Israeli na miaka 40 baadaye (70 B.K) hukumu ikaja. Ndivyo Bwana.
YONA
- Yona (Njiwa) Mwana wa Amitai (Ukweli)
- Akiwa na jukumu la kupeleka injili kwa mataifa, aliondoka kutoka Yopa, Alikuwa na chuki dhidi ya mataifa. Waninawi walitubu.
- Yona alionya Waninawi kutubu ndani ya siku 40, au wapate hukumu.
- Yona "alikufa" na kufufuka tena baada ya siku 3.
MAMBO TUNAYOJIFUNZA:
- Hatuwezi kukimbia kutoka majukumu yetu kwa Mungu na kufanikiwa.
- Ni ujinga kufikiria tunaweza kubadili nia ya Mungu.
- Yona alijaribu, lakini alitambua kupitia uzoefu wenye uchungu kwamba "Yeye anafanya kulingana na mapenzi yake katika jeshi la mbinguni, na miongoni mwa wakazi wa dunia: hakuna anaweza kupinga mkono wake, au kusema kwake, Unafanya nini wewe?" (Dan. 4:35).
- Mungu amemuumba mtu na watu wote watapata kutubu.
- Hakuna mtu ana haki ya kuweka kikomo kwa mkono wa Mungu wenye huruma.
-
Ni lazima kuhubiri Neno la kuokoa na si kujificha taa zetu (Mk. 16:15-16).
MAKTABA YA KUREJELEA:
"The Story of the Bible" (H.P. Mansfield)âTol. 5, Nam. 8
"The Goodness and Severity of God" (H.P. Mansfield)âKur.2-50.
MASWALI YA AYA:
- Kwa njia gani Yona alijaribu kuzuia kusudi la Mungu?
- Nini ilikuwa mbaya na tabia ya Yona kwa Waninawi?
-
Tengeneza orodha ya miujiza iliyofanyika katika hadithi ya Yona.
MASWALI YA INSHA:
1. Kwa kifupi toa muhtasari wa hadithi ya Yona. Ni masomo gani tunaweza kujifunza kutoka na maisha ya Yona? Yesu akawaambia watu wa siku zake: "Kizazi kiovu kisicho na uaminifu kinataka ishara; na hakutakuwa na ishara yoyote itakayotolewa, lakini ishara ya nabii Yona."Katika njia gani Yona alikuwa "mtu wa ishara"?