CSSA 3-3-324 - JOHN THE BAPTIST

Swahili

324.    YOHANA MBATIZAJI

"Miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake hakuna aliyezaliwa mkuu kuliko Yohana Mbatizaji"

Malaki alikuwa amewaambia watu wa nyakati zake kwamba “Hukumu ya Mungu” ingekuja na akawaonya kwamba wachache ndio watakuwa tayari Kumpokea wakati Atakuja. Kwa sababu nchi hii iliojaa ufisadi, ilikuwa inapaswa Mungu kumtuma mjumbe kwanza, “Kutayarisha njia” (Mai 3: 1). Miaka mia nne ya ukimya kwa upande wa Mungu ilisababisha umaskini wa kiroho uliotabiriwa. Ukimya huu ulivunjwa kwa kutokea kwa Ghafla kwa Gabrieli kwa Zekaria. Baadae, kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji, mhubiri wa Masihi, kulileta marekebisho ya Kidini jinsi dhamira ya taifa ilibadilishwa na tabia ya nabii wa nyikani. Kwa njia hii nyoyo za watu zilitayarishwa kupokea “mjumbe wa agano", Mwana pekee wa Mungu.

Lengo letu katika somo  hili ni kuona jinsi Mungu alitenda katika wakati ulioteuliwa kutayarisha wanadamu kwa kuja kwa Mwana wake.

Luka 1:1-27, 57-80
HALI ILIVYOKUWA ISRAELI WAKATI YOHANA ALIZALIWA.

Wakati Warumi walikuja Yudea na kuteka Yerusalemu, waliponda roho ya unafsi na ya utaifa ya Waisraeli ambayo walikuwa wameendeleza katika kipindi cha mamia ya miaka ya utawala wa Wamakabayo. Sasa waliguna chini ya kisigino cha chuma cha ROMA na walitamani kupata Mwokozi. Utumwa wao kwa Roma ulikuwa nembo ya utumwa wao kwa dhambi. Ibada ya taifa ilikuwa imeharibika na kubadilisha taifa likakosa utu na fadhila kwa wengine. Kulikuwa na ufisadi katika sehemu za juu, matajiri na wenye ushawishi mkubwa waliendeleza utawala wao, kwa kujipendekeza kwa mabwana wao wa Kirumi au kwa udanganyifu na unafiki. HERODE MKUU, Mwedomi akageukia dini ya Kiyahudi, alikuwa mkatili na dikteta kwani alifurahia kuonyesha nguvu zake katika kunyanyasa Roma. Ukuhani ilikuwa mikononi mwa Wasadukayo.  Walikuwa na utajiri wa hazina za Hekalu,  walipenda vitu vya dunia na waliishi kwa sasa. Jinsi walivyokuwa hawafai kuwa “wajumbe wa Bwana wa Majeshi” inaonekana kwa kukubali kwao kwa vitabu vitano pekee vya Musa na  wakapinga maisha baada ya kifo- walisema kwamba “hakuna ufufuko, wala malaika wa roho” (Mdo 23: 8). Mafarisayo, tofauti na  Masadukayo, walikubali Sheria, Zaburi na Manabii. Waliipa umuhimu sawa Sheria Simulizi, au "mapokeo ya wazee", ambayo ilikuwa ufafanuzi wa Sheria ya Musa iliotengenezwa na kwa ajili ya kujifunza na Waandishi, au Wanasheria kama Hileli na Shamai (Mt. 15: 2).

Katika mwanzo wao, mabaki wa Israeli waliokuwa wamerudi kutoka uhamishoni walijitenga na Mvuto wa Kigiriki kati ya taifa na  walikuwa na utaifa. Lakini jinsi muda ulivyosonga walikumbatia philosphia ya Wagiriki ya kutokufa kwa roho. Pia umakini wao kwa  maelezo na Barua  ya Sheria iliwapelekea kukosa roho yake. Kwa mtazamo wao uadilifu ulihisisha uzingatiaji kamili wa barua ya Sheria. Hivyo “maswala yenye uzito”, kama “haki, huruma na imani" hayakuzingatiwa sana (Mt. 23:23). Unafiki na kukosa utu ndio matokea ya ibada ambapo wanadamu wanajali wenzao zaidi ya wanavyomjali Mungu (Yn. 5:44).

Pia kulikuwa na makundi ya Kisiasa kama vile kikundi cha Herode (ambaye alifuata familia ya Herode) na zealots (ambao walikuwa wachochezi na walisumbuka chini ya ukandamizaji wa Roma) na hata hivyo katikati ya harakati hizi za kutatanisha, kulikuwa na watu kama Zekaria na mke wake, Elisabeti, ambao walitamani wokovu wa Israeli kwa ujio wa masihi wake.

GABRIELI ANAMTEMBELEA ZEKARIA HEKALUNI (Luka 1:5-25).

Zekaria alikuwa mmoja wa kikundi cha Abia, ambacho kilikuwa moja kati ya amri ishirini na nne ya wana wa Haruni ilioanzishwa na Daudi kuchukua zamu katika huduma ya nyumba ya Mungu  (Mst.5. 1 Nya. 24:10) . Yeye na mke wake walikuwa watumishi wa Mungu waliojitolea na walifuata amri.

Maisha yalikuwa yamewaletea sikitiko moja kubwa – hawakuwa na watoto- ingawa walikuwa wameomba kwa ajili yao mara kwa mara (Mst.13) Bila wao kujua, Mungu alikuwa amewahifadhi kuwa wazazi wa kuhani mkuu zaidi ya makuhani wote atakaye tayarisha njia ya Mwana Wake.

Kila moja ya kozi ishirini na nne za familia ya Haruni walishughulikia Yerusalemu kila moja katika wiki yake.  Kila Kozi iligawanywa mara saba na kila sehemu ilitumikia siku yake katika Hekalu- makuhani binafsi walipewa  kazi katika huduma. Kundi la Zekaria “lilikuwa la kuchoma uvumba”. Hii ilifanyika asubuhi na jioni, na  wakati kuhani aliingia katika Mahali Patakatifu kengele ilipigwa na kimya kingetamba juu ya umati wa wafuasi walioko nje. Uvumba uliokuwa unanukia vizuri ulipaa kutoka kwa madhabahu ya dhahabu, ilikuwa kama sala ya watakatifu  ambayo shukrani na  sifa zilitolewa (Taz. Zab 141:. 2; Ufu. 5: 8; 8: 3). Wayahudi walikuwa wanajua maana ya kiroho ya uvumba wa manukato, kwani tunasoma kwamba  walikuwa “wanasali bila wakati wa kufukiza ubani" (1:10).

 

Wakati akiwa katikati ya  majukumu yake, Zekaria alipata ufahamu wa uwepo wa mtu mwingine. Kwa mkono wa kulia wa madhabahu palisimama malaika  wa Mungu,  akiangazwa na mwanga hafifu kutoka kwa  taa zilizokuwa na matawi saba. Inaonekana kwamba alitambua kwamba mtu yule alikuwa malaika, kwani alijawa na hofu. Kimya cha miaka mia nne kilikuwa tayari kuvunjwa na sauti ya Mungu ilisikika tena: "Usiogope, Zekaria, maana dua yako imesikika, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohana". Hakuamini masikio yake wakati maneno ya faraja na umuhimu yalitoka kwenye kinywa cha Malaika mgeni. Yohana inamaanisha "Neema ya Bwana". Huyu atakayezaliwa ataleta mwanzo mpya  ambapo utukufu wa Bwana utawafanya  watu kutubu dhambi zao na kurejesha sheria, hofu na kifo (Rum. 2: 4., Yn. 1:17).

Gabrieli aliendelea kuhusisha ujumbe maalum wa Yohana kama nabii na mtangulizi wa aliye juu. Utume wake ulikuwa kugeuza moyo wa taifa tayari kwa ajili ya Masihi, katika roho ya Eliya (ambaye baadaye kazi yake, ailiashiria ile ya Yohanai (Mst.15-17; 1 Fal. 18:37; Mal. 4: 6).

Ni wazi kwamba baada ya ujumbe huu Zekaria alishangazwa na kutokea kwa malaika na maneno yake. Alitaka uhakikisho wa ahadi hii, hasa kwa sababu yeye na Elisabeti walikuwa wazee. Jibu la malaika lilimtambulisha. Alikuwa  malaika Gabrieli mwenye mamlaka na la muhimu ni kwamba aliweza “Kusimama mbele ya Mungu” Zekaria alipewa ishara, ambayo ishara yake ilionyesha kukemea ukosefu wake wa amani. Angekuwa bubu mpaka maneno ya  ahadi yatakapo timia (Mst. 19-20).

Watu waliokuwa nje walipatwa na wasi wasi wakihofia jambo limempata. Wakati  alitokea kwa mlango alikumbwa na tatizo la kuelezea kuchelewa kwake. Akiashiria kwa mikono yake huku akijitahidi kuelezea mambo ya ajabu, na wakati walipoona kuwa hawezi kuongea walitambua kwamba alikuwa ameona maono. Watu waliondoka katika Hekalu bila kujua, wakitafakari kuhusu mambo ya ajabu yaliyotokea.

Zekaria akaenda nyumbani baada ya utumishi wake.  Kwa mujibu wa maneno Gabrieli, Elizabeti alipata mimba. Marafiki na jamaa walipatwa na mshangao na furaha walipotambua kwamba walikuwa wanatarajia kijana. Gabrieli alikuwa amesema kwamba  watapata furaha kuu na wengi watafurahia kuzaliwa kwake (mst.14). kama muda ulivyopita Elisabethi alijitayarisha kwa tukio la furaha baada ya muda wa kawaida mtoto aliwasili.
 

KUZALIWA KWA YOHANA MBATIZAJI (Luka 1:57-66)

Neno la Mungu kwa mara nyingine lilidhibitishwa wakati Elisabethi alijifungua kijana. Elizabethi na Zekaria sio pekee waliofurahia jambo hili, kwani pia wakaazi wote wa miji katika milima walifurahia. Walijua jinsi wana-ndoa hawa wawili walivyo tamani kupata watoto na  sasa tamaa yao ilikuwa imetimia.

Katika siku ya nane  majirani na mabinamu  walikusanyika kushuhudia tohara na kupewa jina kwa mtoto. Tohara rasmi iliwajumlisha waume wa Kisraeli katika agano na umuhimu wa kukatwa kwa njia za kimwili. Mtoto huyu angeweza kukata tamaa za kimwili (Mwa. 17:. 13-14; Gal. 5:24). Aidha angewaongoza wengine katika  njia ya kutubu, kukiri na ubatizo- umuhimu halisi wa tohara (Kol. 2: 11-12; Rum. 2:29.).

Wale waliokuwepo walichukua mambo mikononi mwao na kumpa jina Zekaria. Je, si hili lilikuwa jina la baba yake na jina la waisraeli wengi wenye heshima? Maana yake, “Bwana amekumbuka", lilionekana sawa pia. Lakini mapenzi ya Elisabethi hayakuwa yametimia kwani alisema kuwa mtoto angeitwa Yohana. Hili lilileta upinzani mkubwa, alienda kumwomba Zekaria msaada. Hakuelewa upinzani aliokuwa nao mumewe na hakuweza kunena. Walikuwa na uhakika kwamba angedhibitisha chaguo lao, alichukua kibao na kuandika “Yohana”, walishangaa. Kwa udhibitisho wa  uamuzi wake, wakati huo ghafla kinywa chake kikafunguka na akacheka na kumsifu Mungu. (Mst.64). Watu walishangazwa na matukio haya ya ajabu na bila shaka wengi wao walikumbuka matukio haya kwa miaka mingi baadaye. Kwa hivyo kutoka umri mdogo Yohana akawa chombo cha udadisi kama vile watu walivyoshangazwa naye “ Je atakuwa mtoto wa aina gani?” (Mst. 65-66).

 

HUDUMA YA YOHANA MBATIZAJI (Luka. 1:15-17, 76-80).

Samweli na Eliya walikuwa wameleta mageuzi ya kiroho katika Israeli na kazi zao zilikuwa zinafana na za Yohana. Samweli alikuwa mwamuzi wa mwisho na “alitayarisha” kwa ajili ya wafalme kutawala badala yake. Elia pia alikuja mbele ya Ahab baada ya mageuzi ya Karmeli (1 Fal. 18:46). Katika njia zote  manabii hawa wawili wakuu walimtangulia Yohana, kama kumbukumbu ya masomo ya awali yanatuonyesha (Hatua ya 2, Somo la 15 na Hatua ya 3, Somo la 10).

Isaya alikuwa nabii wa kwanza kuongea hasa kuhusu nabii wa Jangwani, “ Sauti yake inayolia jagwani, tengenezeni njia ya Bwana” (40:3-8).  Aliendelea akitumia lugha ya taswira kuonyesha vile hili lingetendeka. Njia zilizo kombo za wanaume  lazima  zingenyooshwa na “Milima” ya kiburi cha binadamu lazima ingefanywa kuwa tambarare katika sura ya utukufu wa Mungu ambapo ulikuwa tayari  kufunuliwa.  “miili yote”  bila kujali msimamo wa kijamii,ilikuwa kama nyasi na haingeweza kupinga Roho wa Bwana uliovuma juu yake. Wote walioishi “kwa kila neno litokalo kinywani mwa Bwana” pekee “Watasimama Milele”. Nabii wa jagwani hangekuwa na mapendeleo, Tajiri au maskini, mwema na asiye mwema, angehimizwa kubatizwa baada ya kukiri dhambi zao, kama walitamani kupokea ondoleo la dhambi zao.

Malaki, akitumia maneno sawa na Isaiya, alitangaza kwamba “mjumbe wa agano", lazima atanguliwa na yule atakaye "tayarisha njia” (3:1 Kwa njia gani wangeweza kusimama katika siku yake ya kuja? Waandishi wa injili wanarejelea Isaya 40 na Malaki 3 wakati wanaelezea utambulisho na huduma ya Yohana (1 mfano Mk. 2, 3).
 

Wakati Gabrieli alimjia Zekaria alitaja tabiri zote mbili na kuongeza maelezo zaidi. Alitangaza kwamba Yohana Mbatizaji atakuwa mkuu mbele ya macho ya Mungu kwa sababu ya kujitolea kwake kwa Mungu pekee. Kama Mnadhiri, hakuna mvinyo au kileo kilipaswa kuzubaisha akili yake. Zaidi ya hayo huduma yake ilikuwa takatifu kwamba hata akiwa katika tumbo la mamake Roho Mtakatifu ulijaa ndani yake. Hivyo akiwa na kipaji aliweza kwenda akiwa na uamuzi sawa na wa Eliya, na kuwageuza wote wale ambao wangesikiza ujumbe wa Mungu wao.  Huduma yake ilifanana na ile ya Eliya na hii inaonekana kwa ukweli kwamba manaeno yaliyotumiwa juu ya jukumu inayokuja ya Eliya katika kurudi kwa Kristo, yametumiwa na  Yohana (Taz. Lk 1:.. 16-17; Mai 4: 6). Hakika angekuwa kama “Eliya” wa kizazi hicho (Mt.17:12).

Baada ya Zekaria kuongeleshwa na Roho kuhusu kazi ya Messia (Mst. .67-75), alinena na mwanawe (Mst.76-80) Alinena na yeye kama “nabii wa Mungu Mkuu” ambaye “ataenda mbele ya uso wa Mungu” na kuleta “maarifa ya wokovu" kwa watu wake. Ilikuwa ni upendo na mshangao zilizomjaa Zekaria alimwangalia mwanawe mpendwa. Kisha kwa maneno ambayo yanayokumbusha maana ya jina lake,  alitangaza kwamba wokovu  kama huu ungekuja kupitia msamaha, kwa sababu ya huruma ya Mungu ya kumtembelea mtu.

"Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni, Alikaa jangwani mpaka siku alipojitokeza rasmi kwa watu wa Israeli.” (Mst.80). kwa upweke, akiishi kwa kula nzige na asali ya mwitu, alikua na kuwa mtu mzima. Mbali na ufisadi wa mawazo ya kisasa, akishughulika sana na fikra za mambo ya kiroho, Yohana alisubiri mpaka wakati ambao Mungu  angemtuma kwa huduma yake kama mtangulizi wa Masihi. Angeweza bila woga kupatia dhamira ya taifa changamoto na kuwarudisha watu kwa Mungu.

 

MAMBO TUNAYOJIFUNZA:

  • Kwa muda uliopangwa Mungu alivunja ukimya wa miaka 400 ili kuandaa watu kwa ajili ya kuja kwa Mwana wake.
  •  Mungu anataka sisi tumpenda kwa moyo wetu wote, nafsi na akili. Lakini ibada ya Israeli ilikuwa imezorota na kugeuka kuwa hali ya ubinasi na kukosa utu. Hivyo badala ya kuwa wanyenyekevu wakawa wenye kiburi, na wanafiki.
  •  Elisabeti na Zekaria walikuwa  wazee na Elisabeth alikuwa amepita umri wa kuzaa. Hata hivyo hawakujua kusudi la Mungu, ambalo liliwahitaji kuwa na mwana katika umri wao mzee ambaye anapaswa kuandaa njia ya Bwana.
  • Mbali sana na anasa za maisha na anasa za kidunia, Yohana ilikuwa ameelimishwa kwa kazi ngumu ya kuandaa watu kwa ajili ya Bwana. Katika mazingira kama hayo alijifunza kumtegemea Bwana na alipata nia kali ya kujitolea iliomwezesha kutimiza kazi yake.

 

MAKTABA YA KUREJELEA:

"The Ministry of the Prophets" (C.C. Walker)—Sura. 40

"Nazareth Revisited" (R. Roberts)—Sura 4 - 5

"The Story of the Bible" (H.P. Mansfield) — Tol. 8, Nam. 1

 

MASWALI YA AYA:

  1. Kumbuka tukio ambapo Yohana Mbatizaji alipewa jina.
  2. Je, nini Gabriel alimwambia Zekaria kuhusu mwanawe Yohana alipokuwa katika hekalu?
  3. Je, nini unajua kuhusu malezi ya Yohana Mbatizaji? Je alikuwa Mtu wa aina gani?
  4. Tengeneza orodha ya kufananisha Yohana Mbatizaji na Eliya?
     

MASWALI YA INSHA:

  1. Eleza hali ilivyokuwa Israeli wakati Yohana Mbatizaji alizaliwa. Nani waliokuwa viongozi na ni makundi gani ya kidini yalikuwa huko?
  2. Simulia mazingira ya kuzaliwa kwa Yohane mbatizaji.
  3. Orodhesha huduma ambayo Yohana mbatizaji aliitwa kufanya.
  4. Jinsi gani unaweza kulinganisha kazi iliyofanywa na Elia na Yohana Mbatizaji?
  5. Ni hatua gani Mungu alichukua kuandaa ulimwengu kwa ajili ya kuja kwa Mwana wake?

 

 

Swahili Title
324. YOHANA MBATIZAJI
Sub type
Sub sub type