339

Swahili

339. UPINZANI UNAKUSANYIKA KATIKA KIVULI CHA MSALABA

"Lazima aende Yerusalemu na apate mateso mengi . . . na kuuawa"

Mwaka wa mwisho wa Bwana ulikuwa na uzindisho wa uchungu kama alivyoendelea kwa njia ambayo ingeelekea  kwa kifo chake. Shinikizo la upinzani zilikuwa zinaongezeka dhidi yake na tunamwona kama “Aliyedharauliwa na kukataliwa na binadamu; mtu wa huzuni na matatizo”.

Hata, hivyo yeye aliwajali wanafunzi wake, nia yake ya kuwaelekeza na kuwatayarisha kwa ajili ya sadaka waliopaswa kutoa. Huu ni mfano wa hali ya ubinafsi ambayo inapaswa kuelekeza huduma yetu.

Lengo la somo hili ni kuonyesha kuwa mateso huja kabla ya malipo-kwa Masihi pamoja na wanafunzi wake.

MATHAYO 16


MAFARISAYO NA MASADUKAYO WANAHITAJI ISHARA (Mt. 16:1-4).

Ilikuwa muda tangu Yesu alikutana na Mfarisayo. Alikuwa amewaacha baada ya mjadala kuhusu unajisi (Mt. 15), na kusafiri kaskazini, mbali na ushawishi wao, na kisha hadi Galilaya sehemu ya Dekapoli katika kingo za mashariki mwa Galilaya.

Punde tu Yesu alivyovuka ziwa kwa upande wa kingo za Magharibi alipewa changamoto kutoka kwa kundi la Mafarisayo na Masadukayo (Mt 15:39, 16: 1).  Baada ya matukio yake ya kuchangamsha na Watu wa Mataifa, kukabiliana na kundi hili kuliashiria kwa Bwana kwamba muda wa mwisho wa upinzani ulikuwa tayari kuanza. Kuanzia sasa angekuwa akitembea katika kivuli cha msalaba.

Uwepo wa Masadukayo mbali na Yerusalemu ilikuwa ishara ya wasiwasi ambayo Yesu alikumbwa nayo. Zaidi ya hayo, Masadukayo kwa kawaida hawakupatikana pamoja na Mafarisayo (Linganisha Mdo 23: 7) lakini kama Herode na Pilato, wangekuwa marafiki wakati kulikuwa na kazi ambayo uadui wao dhidi ya  jambo pamoja ungetukuzwa.

Walimwamuru Yesu awape ishara kutoka mbiguni ambayo ingetumika kudhibitisha ujumbe wake kati yao. Hii ilionekana kama madai ya kawaida. Musa alikuwa ametoa ishara kama hio (Kut. 4: 1-9). Pia Yoshua (Yos. 10: 12-14), Samuel (1 Sam 12: 16-18), na Eliya (1Fal. 17: 1).

Lakini ni ishara gani ingekuwa na umuhimu wowote kwa wale waliopuuza ishara kama kuponya wagonjwa, kufufua wafu, kuwapa vipofu uwezo wa kuona na kufungua masikio ya viziwi (linganisha Mt 11:4-5) Ni ishara gani ingetolewa kwa mafarisayo waliojaa ubinafsi na hawakuona utakaso wa roho kama sharti la utakatifu au Masadukayo wanafiki ambao walikataa dhana ya ufufuo? Watu hawa wanafiki, walikuwa wanamjaribu Mungu.

Katika matukio kama haya, Yesu alikuwa amekataa ombi lao (Yn. 2:18, 6:30; Mt12:38) badala yake wangepokea “ishara ya nabii Yona”
 

ISHARA YA NABII YONA

Maneno ya Yesu yalirejelea ujumbe na huduma ya Yona. Baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu,  aliwapa watu wa Ninawi siku arobaini kutubu ama uharibifu ungeshuka kwa mji wao. Waninawi walitubu na adhabu iliotishiwa ikaepukwa. Lakini Yesu, alitaja kizazi hiki kama “ Kiovu na kisherati”, kuonyesha kwamba hakungekuwa na toba kwa hivyo adhabu ingekuja.

Ishara zilikuwa wazi kama tu Mafarisayo na Masadukayo wangefungua macho yao kuona ishara hizo. Walitazama mbiguni asubuhi na jioni na kulingana na rangi ya anga wangetabiri hali ya hewa. Hawangeweza kuinua macho yao na kuona ishara za dhoruba ijayo?

Ujumbe kwao ulikuwa onyo! Yesu aliwaambia kwamba hawatapata ishara yoyote “ila tu ishara ua nabii Yohana”. Hii ilikuwa ishara ya ufufuko baada ya siku 3(Mt 12:40). Lakini ishara ingekuja baada ya sadaka yake kwa mikono yao! Hivyo ingedhibitisha hatma yao na wengi wangekuwa wamechelewa.

"Kama wao hawaamini Musa na manabii, hawatashawishiwa na hata mtu akifufuka katika wafu” (Lk. 16: 30-31). Walibaki bila kutubu na katika miaka arobaini majeshi ya Kirumi yalimwaga damu ya Kiyahudi. Yesu “akawaacha na kuondoka”. Nafasi ilikuwa imepotea. Yesu hangewalazimisha kupokea neema ya Mungu kwa watu wasio ihitaji.


CHACHU ZA MAFARISAYO NA MASADUKAYO (Mt. 16:5-12)

Chama kidogo kiliondoka Magdala kwa haraka kwamba wanafunzi walisahau kununua mikate. Walipofika upande wa pili Yesu aliwaonya kuhusu chachu za Mafarisayo na Masadukayo. Alikuwa anatafakari yale ambayo chuki za adui zake zingesababisha na alijua kwamba mmoja wa wanafunzi wake angegeuzwa dhidi yake. Lakini, kama ilivyotokea mara nyingi, walishindwa kumwelewa na ilibidi waelezewe kwamba kile alichokuwa akitafakari siyo "chachu ya mikate, bali mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo."

Kama chachu inavyopenya katika unga mpaka mchanganyiko wote unajaa chachu, hivyo upinzani wa Yesu ulikuwa unaenezwa na maadui wake katika taifa.

Lakini Yesu alimaanisha nini kwa "chachu ya Mafarisayo na Masadukayo." Hakuongea kuhusu chachu  ya kila moja, bali chachu iliyokuwa kwa wote. Vilikuwa vyama tofauti.

  • Chachu ya Mafarisayo ilikuwa unafiki (Lk 12: 1). Walikuwa wakali, waliojaa na uzalendo na walioshughulika na tabia za sheria. Hili walitenda kama mchezo wa kuigiza, “waonekane na wanadamu”.  Nyoyo zilishughulika na sifa kwa binadamu na sio zifa kwa Mungu (Mt 5: 5, Yn. 05:44).
  • Chachu za Masadukayo zilikuwa utajiri. Hawakujali dini yao na walijali tamaduni za nje na mambo ya dunia. Hawakuamini ufufuo au zawadi ya siku za usoni na walikuwa katika faida ya sasa. Bila aibu walipokea sadaka ya hazina ya Hekalu.

Ingawa Mafarisayo na Masadukayo walitofautiana, waliungana kwa ajili ya uadui dhidi ya Yesu na walitaka ishara yake. Wote hawa walikuwa wametoka katika “kizazi kiovu kisicho na uaminifu". Hili ndilo muhimu ya chachu kwa wote. Yesu aliwakilisha mambo ya Mungu. Walikuwa waovu,waliojaa ubinafsi na waliokufa kwa Mungu. Jambo tunalojifunza ni kwamba chachu bado inaenea, unafiki na kupenda mali bado vipo ulimwenguni. Waliungana katika chachu za uovu ambazo zinaweza jaza maisha yetu na kutuondoa kwa Kristo

KUKIRI (Mt. 16:13-16)

Kutoka Galilaya Bwana aliwaongoza wanafunzi wake kaskazini kuelekea Kaiserea Filipi. Sasa ilibidi awatayarishe wafuasi wake kwa ajili ya mateso na kifo chake. Katika ukimya wa mlima aliwauliza, "Watu wanasema kwamba mimi, Mwana wa mtu, ni nani?". Jibu lao lilionyesha upungufu wa jinsi watu walivyomchukulia Yesu. Wakati mmoja walikuwa wanatilia shaka kwamba alikuwa Mesihi (linganisha Yn. 6: 14-15), lakini jibu la wafuasi wake lilionyesha kwamba alikuwa ameshindwa kulingana na mtizamo wa watu wa Masihi- upinzani dhabiti ulikuwa umebadilisha mtizamo wao na sasa walimchukulia kama tu “mmojawapo wa manabii” (Mst14).

Lakini swali la Bwana lilikuwa la muhimu kwani liliongozwa na uchunguzi wa mkuu, “lakini nyinyi mnasema mimi ni nani? (MST 15).

Petro ndiye aliyejibu, "Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai." Huu ulikuwa wakati wa kufurahi wa Yesu, kwani licha ya yote yaliyokuwa yametokea yakumkana Yesu, Petro alitambua kwamba alikuwa Mesihi. Yesu alimpongeza, “heri iwe nawe, Simoni mwana wa Yona, kwa maana ya damu na nyama havikufunulia haya, bali ni Baba yangu, aliye mbiguni” (Mst17).

Wewe Simoni, mwana wa Yona " inaelezea ukoo wa kidunia wa Petro- na ukweli kwamba alieleza Yesu kama "Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai," ilionyesha Mungu alikuwa akifanya kazi katika maisha ya Petro- alikuwa mtoto wa Mungu (Yn. 1:13). Katika aya ya 18 Yesu aliendelea na kusema, “Nami nakwambia, ewe Petro ('Petros') juu ya mwamba huu (‘petra’) nitajenga kanisa langu, na milango ya kuzimu haitalishinda".  Katika kukiri kwake Petro alikuwa amedhibitisha uchaguzi wa jina lake jipya na Bwana » (Yn. 01:42). Ilikuwa Petro ambaye alielezea katika waraka wake wa Eklezia kama kanisa lililojengwa juu ya jiwe kuu la pembeni, Bwana Yesu (1Pet. 2 5-6).

Kwa mara ya kwanza katika injili ya Yesu alitumia neno "Iklezia" kwa mfuasi wake, tofauti na masinagogi ya Kiyahudi. Hivyo katika wakati ule, wakiwa mbali na Hekalu na ibada za Kiyerusalemu, kiongozi aliyekataliwa pamoja na kundi lake dogo la wakimbizi walitangaza ushindi wa Eklezia- "milango ya kuzimu haitalishinda”.

Bwana alielezea kwamba Petro angepewa “funguo za ufalme” na kwamba maamuzi yake yaliyofanywa kwa imani yangepokea nguvu za Mungu- nguvu ambazo baadae ziligawanywa kwa mitume wote (Mt. 18:18). ufunguo ulikuwa beji ya ofisi au mamlaka (Isa. 22:22), kwani  mtu aliyekuwa na ufunguo huu alimiliki ruhusa ya kuingia kwenye jego hili. Ilisemwa katika kuwahukumu Waandishi kwamba “walikuwa wamechukuaufungua wa wa maarifa" (Lk. 11:52). "Funguo za ufalme" kwa hivyo zilielezea nguvu za kufungua hali ya kuelewa  nafasi ya kweli  ya Bwana Yesu Kristo na binadamu, ambapo njia ya Ufalme wa Mbiguni ingepatikana. Lakini Petro alikuwa shughuli maalum katika utumizi wa funguo. Yesu alimwita “Simoni Bar-Yona” au Simoni mwana wa Yona. Ilikuwa ni kama vazi la nabii mkubwa Yona lilikuwa limewekwa katika mabega ya Petro. Ingekuwa jukumu lake kueneza injili kwa Wayahudi (kama alivyofanya katika kukiri wokovu katika jina la Yesu Kristo-Matendo 2 na 3), na baada ya kusita kwa awali katika kuelewa, kufungua mlango wa imani kwa Watu wa Mataifa (katika mwito wa Korneli-Matendo 10).

vazi la nabii mkubwa Yona imeanguka juu ya mabega Petro. Itakuwa wake kufungua Injili kwa Wayahudi (kama alivyofanya kwa kutangaza wokovu katika jina la Yesu Kristo-Matendo 2 na 3), na baada ya kusita awali kutokana na kushindwa katika akili, kufungua mlango wa imani Mataifa (katika mwito wa Cornelius-Mdo 10).

 

MAELEZO KATIKA NJIA YA MSALABA (Mt. 16:20-27)

Juu ya misingi ya kukiri kwa Petro Yesu aliweza kuwaonyesha asili ya Umasihi wake na pale itakapo mpeleka: “Tangu wakati huo Yesu alianza kuwajulisha waziwazi wanafunzi wake, kwamba lazima angeenda Yerusalemu na kuteseka kwa mambo mengi katika mikono ya makuhani wakuu na Waandishi, na kuuwawa na kisha kufufuliwa tena katika siku ya tatu.” Kuteseka hakukuwa kigezo cha Umasihi wake lakini udhibitisho wake kwamba “Masihi mkuu” atauwawa (Dan 9: 25-26).

Ilikuwa ni utumizi wa maneno mazito na Yesu kama (“lazima....kuteseka...kuuawa”) ambayo yalileta majibu ya Petro. Ufunuo wa Messia aliyekataliwa na anayeteseka ulimzidi. Upendo wake kwa Mola wake ilikuwa mkubwa mno kukubali picha hii ya kutisha ya kuteswa na kifo. Akapinga na kusema “Hasha Bwana, hayo hayatakupata”. Lakini upendo huu ulikuwa kikwazo kwake na kwa Bwana wake.Yesu angeweza kustahimili chuki za adui zake kuliko upendo potofu kutoka kwa marafiki zake. Alikataa majaribu ambayo Petro alikuwa ameweka mbele yake, akitumia maneno sawa na yale aliyomwambia mshawishi wakati alipomweka katika majaribu kama haya hapo awali, “Nenda nyuma yangu, Shetani;  wewe ni kikwazo kwangu, kwa maana huyawazi yaliyo ya Mungu, lakini yale yaliyo ya binadamu”( Mst 23; linganisha Mt 4: 8-10).

Kifo cha Yesu kilikuwa muhimu kama alikuwa “atimize haki yote” (Mt. 3:15;. Rejelea somo la 2); hili lilikuwa tendo la utiifu (Flp. 2: 8-9). Bila msalaba hakungekuwa na taji- kama hangeteseka hakungekuwa na utukufu.

Yesu alitumia kunguka kwa Petro kuonyesha wafuasi wake nafasi yao katika nia ya Mungu. Msalaba ambao ulikuwa umesababisha kilio kutoka kinywa cha Petro ungekuwa mzigo Wafuasi wake pia! “ kama mtu yeyote anataka kunifuata mimi, lazima ajikane mwenyewe, achukue msalaba wake na anifuate” (Mst.24). Maisha yao kama wanadamu wanaomfuata lazima yawe maisha ya kujitolea, kujinyima tamaa za mwili na kutamani mambo ya Mungu. Alikuwa amekuja kuwapa uhai. Kukubali zawadi hii kungemaanisha kupoteza zawadi zote zingaazo za dunia.

Lakini Yesu aliendelea: Kwani yeyote atakaye kuikoa nafsi yake ataipoteza; na yeyote atakayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataipata”. Kwa maana “hasara” zipatikanazo katika maisha haya kwa ajili ya huduma ya Yesu, hatimaye yatapatikana kama maisha yenye dhamani kubwa kuliko ushindi wa sasa wa dunia (Mst. 26). Wale ambao maisha yao yamejaa na hali ya kujifurahisha na kujitosheleza watayapoteza yote.

Katika maneno yake ya mwisho Yesu aliweka matumaini yake ya Kimesihi katika mtizamo unaofaa. Walikuwa haki kutarajia mfalme ambaye atakuja na nguvu za kuokoa Israeli. Lakini mateso lazima yaje kabla ya zawadi- kwake na kwao pia. Maneno haya yanatumika hadi leo kama yalivyotumika wakati huo.

MAMBO TUNAYOJIFUNZA:

  • Ishara tunazo kuona katika ulimwengu za kuipindua kwa ustaarabu wa kisasa ziko wazi kama ishara ya Mafarisayo na Masadukayo waliona, na kupuuza. Ni jukumu letu kupambanua.
  • Chachu za Mafarisayo (unafiki), na chachu ya Masadukayo (utajiri) bado zipo na zinachanganyika na chachu ya uovu ambayo inaweza kututenganisha na Kristo.
  • Kukiri kwamba Yesu ni "Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai" ni msingi ambao Iklezia imejengwa juu yake.
  • Kama Masihi alishiriki mateso, hivyo uanafunzi lazima uhusishe sadaka.

 

MAKTABA YA KUREJELEA:

"A Life of Jesus" (M. Purkis)—Kitabu cha 5, Sura 6-8

"The Gospel of the Son of God" (L. G. Sargent)—Sehemu ya Nne, Sura

3-4 "The Story of the Bible" (H. P. Mansfield)—Tol. 9, Kurasa 149-166


MASWALI YA AYA:

  1. Ni makosa gani walitenda Mafarisayo na Masadukayo kwa kuuliza Yesu atoe ishara walipokutana naye katika Magdala?
  2. Nini ilikuwa chachu ya Mafarisayo na Masadukayo ambayo Yesu aliwaambia wanafunzi wake watahadhari?
  3.  Kwa nini kukiri kwa Petro kulikuwa muhimu kwa Yesu?
  4. Yesu alimaanisha nini aliposema, "Kila mtu anayetaka kuokoa maisha yake, atayapoteza" (Mt. 16:25)?
  5.  Kwa nini ilibidi Yesu kufa ili awe Masihi?

MASWALI YA INSHA:

  1. Simulia tukio ambapo Petro alikiri: "Wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai." Kwa nini maneno haya yalikuwa muhimu sana? Kwa njia gani Petro alitumia funguo za Ufalme?
  2. Jinsi gani Yesu aliwaandaa wanafunzi wake wakati alikabiliwa na ongezeka la upinzani na kukaribia kwa kifo chake?
  3. Eleza hadithi ya  kukiri kwa Petro na uelezee maneno ya Yesu ya pongezi.
  4. Kwa nini Yesu alimwambia Petro, "Ondoka mbele yangu, Shetani" (Mt. 16:23)?

 

 

Swahili Title
339. UPINZANI UNAKUSANYIKA KATIKA KIVULI CHA MSALABA
Sub type
Sub sub type