CSSA 2-1-09 - THE HOPE OF THE PROMISES MADE UNTO THE FATHERS

134. TUMAINI LA AHADI WALIZOPEWA MABABA
Tumejifunza maelezo ya historia ya maisha ya Ibrahimu. Na sasa tutaangalia mafundisho kutokana na ahadi kubwa na za thamani alizopewa mtu huyu mkubwa mwenye imani, na akapewa Isaka na Yakobo.

Kusudi la somo hili ni kuona umhimu wa ahadi hii kwa Ibrahimu ikiwa ni ya pili kati ya maagano matatu ambayo katika haya ndiyo msingi wa makusudi ya Mungu. Agano la kwanza lilifanyika katika bustani ya Edeni ambapo ahadi ilitolewa ya uzao wa mwanamke ambaye atashinda dhambi na kifo (Mwanzo 3:15).