Correspondance Course - Lesson 60

Somo la 60

HATUA INAYOFUATA

Somo: Matendo 2

Imekuwa ni furaha kushirikiana nawe katika kozi hii ya kujifunza Biblia. Kwa sasa tumefikia mwisho wa masomo haya, na pengine unajiuliza: Nini kinafuata, au kitu gani nifanye? Kabla hatujajaribu kukusaidia kwa maswali haya, ni muhimu kukumbuka kozi hii ni kwa ajili ya nini. Tumekuwa tukikuonesha mafundisho ya msingi ya Biblia.

Correspondance Course - Lesson 58

Somo la 58:

NEEMA YA MUNGU

Somo: Wafilipi 3

Tunavyokaribia mwisho wa kozi hii, inafaa tuyaangalie masomo yote na kukumbuka kile ambacho tumetaka kukipata. Tumeona kutoka katika Biblia kuwa, maisha mapya katika Kristo ni tofauti sana na maisha watu wanayoishi kabla ya kubatizwa. Ufuasi unataka kujizatiti kuufuata mfano wa Bwana Yesu Kristo, na anawataka watu wajipime kwanza kabla hawajafanya uamuzi kumfuata. Anasema:

Correspondance Course - Lesson 57

Somo la 57:

IMANI NA KUUFANYIA UKRISTO KAZI

Somo: Waebrania 11

Mara nyingi katika masomo yetu haya, tumetumia neno ‘Imani’. Sasa ni wakati wa kutazama na kuona ni nini waandishi katika Biblia wanachotutaka tuelewe juu ya neno hili. Ni neno linaloweza kutumika katika lugha yetu ya kawaida kwa namna kadhaa.

Correspondance Course - Lesson 56

Somo la 56:

ZAWADI YA HALI YA JUU YA TUMAINI KATIKA MAISHA YAKO

Somo: Maombolezo 3

Tumaini ni mojawapo ya zawadi za maana sana zinazotoka kwa Mungu. Kwa upendo wake kwetu, alijua ni kwa kiasi gani mwanadamu angehitaji hili, na kwa namna alivyoushughulikia uanadamu wetu, ametuwezesha kuwa nalo hata katika mazingira yaliyo mabaya sana. Hebu funua Biblia yako usome waraka wa pili wa mtume Paulo kwa Wathesalonike, Sura ya  pili, mstari wa kumi na sita na kumi na saba.

Correspondance Course - Lesson 55

SOMO LA 55

HUKUMU

SOMO: 1 Wakorintho 15

Mojawapo ya njia zilizotumiwa huko nyuma kuwashawishi watu wajiunge na Ukristo, ilikuwa kuwatisha juu ya Kiti cha Hukumu cha Kristo. Kusudi la masomo haya ni kukuelezea faida na haja ya wewe kubatizwa katika Jina la Yesu. Kwa hiyo, ni muhimu tuangalie mada hii ya hukumu, kwa kuipitia mistari inayosemea jambo hili katika Biblia.