Correspondance Course - Lesson 44

Somo la 44

MAISHA YA KRISTO - Eklesia

Somo: 1 Timotheo 3

Wanaume na wanawake wanapobatizwa katika Kristo, wanakuwa watu wa Mungu, na kuwa sehemu ya familia yake. Mungu aliamuru kuwa wanawe wawe katika jumuia ya kiimani, na ametueleza wazi hili liweje. Amepanga kuwe na kundi moja au jumuia moja ya wafuasi kwa dunia nzima. Neno linasema:

Correspondance Course - Lesson 42

Somo la 42

MAISHA YA KRISTO - Dhambi

Somo: Warumi 7

Ulevi wa Dhambi

Kuna nguvu katika maisha ya kila mmoja wetu inayotushinda. Ni ulevi unaozidi ulevi wa pombe, kamari au madawa ya kulevya, nao ni ulevi wa ‘dhambi’. Ni tatizo linalotukamata vibaya; tunakuta tumekosea na inakuwa vigumu kujizuia, na tunavutwa kuendelea hivyo.

Correspondance Course - Lesson 40

Somo la 40

HUDUMA YA KUMEGA MKATE

Somo: Mathayo 26

Katika somo la 31 tuliona kwamba, ubatizo ni mwisho wa maisha yetu ya kwanza, na mwanzo wa maisha mapya katika Kristo. Tunakuwa sehemu ya familia ya Mungu; wanawe wa kiume na wa kike, na kwa hiyo tunakuwa kwa pamoja ni ndugu katika Kristo. Tunakuwa ‘wafuasi’ wa Yesu; neno lenye maana ya ‘wanafunzi’; watu wanaojifunza kumfuata mtu. Tunaweka maisha yetu katika kuyafuata maneno ya Yesu na mfano wake. Mwenyewe alisema:

Correspondance Course - Lesson 39

Somo la 39

UWEZO YA ULIMI

Somo: Yakobo 1

Kiti cha Hukumu

Yesu Kristo atakaporudi kuusimamisha Ufalme wa Mungu, kila mtu aliyeujua na kuuelewa ujumbe wa Injili, ataitwa kumpokea na atahukumiwa naye. Wale ambao wamekuwa waaminifu kwake katika maisha yao watapewa nafasi katika Ufalme huo, na wale ambao hawakuwa, watakataliwa na Bwana na kuondolewa wafe.

Correspondance Course - Lesson 37

Somo la 37

USOMAJI BIBLIA WA KILA SIKU

Somo: Zaburi 119: 89-112

Biblia ni kama kisima kirefu cha maji safi; kisima ambacho kamwe huwezi kukifikia chini kwa jinsi kilivyo kirefu. Hutaweza kamwe kufikia wakati utakapoweza kujisikia umeijua yote kabisa, huhitaji kulisoma tena Neno la Mungu. Hebu ona jinsi baadhi ya watu walivyolipokea Neno la Mungu.

WAYUNANI WA BEROYA                          PAULO

 ALIVYOWAANDIKIA                                  WATHESALONIKE

Correspondance Course - Lesson 36

Somo la 36

KUTEMBEA KATIKA NJIA MPYA YA UZIMA

Somo: Warumi 6

Mwanzo mpya

Tunapobatizwa, tunaanza maisha mapya. Tunakuwa, “tulizikwa pamoja naye (Kristo) katika mauti yake”, wakati tulipotumbukizwa katika maji ya Ubatizo. Maisha tuliyoishi mpaka wakati huo yanakuwa yamefikia mwisho wake; yanakuwa yamepita. Inakuwa:

Correspondance Course - Lesson 35

Somo la 35

MAOMBI

Somo: Zaburi 107

Kuweza kumwomba Mungu wa mbinguni ni fursa tuliyonayo ya kipekee sana. Ni fursa ambayo yeye Mungu ameitoa kwa kila mtu aliye mnyenyekevu, na ambaye anatambua kuwa yeye Mungu ndiye aliyekifanya kila kitu kilichopo duniani. Kuomba/kusali kunaweza kukaonekana kuwa ni kitu kigumu. Sababu ni kwamba, kuna mtengano ulio mkubwa sana kati ya Muumba aliye mbinguni na vitu alivyoviumba vilivyoko katika dunia.