Correspondance Course - Lesson 32

Somo la 32

NDOA YA KIKRISTO

Somo: 1 Wakorintho 7

Ndoa ni makubaliano ya mwanamume mmoja na mwanamke mmoja kuishi pamoja. Haitoshi tu kuwa na ‘kaya’ moja. Watu hao wawili ni lazima wajioneshe hadharani kuwa wanakuwa mume na mke, kwa hiyo makubaliano yao yanafanywa mbele ya mashahidi. Lakini, ndoa na Kikristo si hivyo tu.

Correspondance Course - Lesson 31

Somo la 31

UBATIZO

Somo: Yohana 3

Baada ya kufufuka na kutoka kaburini, na muda mfupi kabla ya kupaa kwenda mbinguni, Bwana Yesu Kristo alisema ifuatavyo kwa mitume wake:

“Enendeni ulimwenguni mwote mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka, asiyeamini, atahukumiwa” (Marko 16:15, 16).

Mambo mawili yako wazi sana katika maneno haya:

Correspondance Course - Lesson 30

Somo la 30

IBILISI NA DHAMBI

Somo: Waebrania 2: 9 - 18

Ni kweli Biblia inamwongelea Ibilisi. Ibilisi ni nini au ni nani? Neno la Kiyunani ni ‘diabolos’. Hebu tuone kama Biblia inaweza kutupa jibu yenyewe.

Katika 1 Yohana 3:8 tunapewa sababu ya Mungu kumtuma Yesu; ni, “Ili azivunje kazi za Ibilisi.” Alidhihirishwa kusudi anayofanya Ibilisi yasiwe yakishinda. Katika Waebrania 2:14 tunaambiwa pia kuwa, Yesu alikuja amharibu Ibilisi na kazi zake.

Correspondance Course - Lesson 29

Somo la 29

IBILISI, MAPEPO, SHETANI

Somo: Mathayo 8:14-34

IBILISI NA PEPO

Kuna maneno mawili ya Kiyunani yaliyotafsiriwa ‘Ibilisi’ katika Biblia zetu, na kwa kuwa yanamaanisha vitu tofauti, tutahitaji hasa kujua kila neno lina maana gani. Maneno hayo ni:

   Daimon – lenye maana ya ‘roho mbaya au roho mwovu’

   Diabolos – lenye maana ya ‘msingiziaji au mchongezi’

Correspondance Course - Lesson 28

Somo la 28

MALAIKA

Somo: Waebrania 1

Malaika ni wajumbe wa Mungu. Wanaweza kuuingia ‘uwepo’ Mtakatifu wa Mungu, kwa hiyo ni sharti wawe viumbe wasio na dhambi. Hatuambiwi malaika wako wangapi, ila tunajua hesabu yao ni kubwa kwa kusoma Waebrania 12:22, na Mathayo 26:53.

Malaika wanafanya nini?

  • Wanatoa ujumbe
  • Wanaongoza
  • Wanafanya ulinzi na kuokoa
  • Wanaangamiza

Tutaviangalia vipengere hivi kimoja-kimoja:

Correspondance Course - Lesson 27

Somo la 27

UZIMA WA MILELE

SOMO: Yohana 3

Utakuwa umekwishaona katika mafundisho haya ya Biblia ya kwamba, mwanadamu wa kwanza, Adamu, aliumbwa kwa Mungu kuutengeneza mwili kwa udongo, na kisha kuupulizia pumzi ya uhai. Lakini, Adamu na Hawa walikosa, na hivyo walibadilika na kuwa viumbe vinavyokufa.

Watu wote, wanaume kwa wanawake, hatimaye wanakufa, kwa kuwa wote wanakosa; ni wadhambi. Ni kitu kisichokubalika mbele ya Mungu, kwa wadhambi kuishi milele. Haiwezekani!

Correspondance Course - Lesson 26

Somo la 26

HUKUMU

Somo: Mathayo 25

Ni lazima kumtii Mungu

Mfalme Daudi alipokuwa amekikalia ‘kiti chake cha enzi’ katika jiji lake la Yerusalemu, aliazimia kulirudisha Sanduku la Agano la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu, lilipokuwa limekaa kwa muda. Mkokoteni ulitegeshwa wa kukokotwa kwa mnyama. Yote yalipokuwa yametengemaa, makuhani wa Mungu walitembea kando-kando la hilo sanduku lilivyokuwa likivutwa.

Correspondance Course - Lesson 25

Somo la 25

UFUFUO KUTOKA KWA WAFU

Somo: 1 Wakorintho 15

Neno ‘Ufufuo’ maana yake ni kuwa hai tena

Lazima lilikuwa ni tukio zuri sana la ajabu kuliko yote katika historia ya dunia, Yesu alipotoka kwenye kaburi lake, baada ya kuwa mfu kwa siku tatu. Wanafunzi wake walipomwona, hawakuweza kuyaamini macho yao. Walifikiri wanachokiona ni roho, lakini Yesu aliwaambia: