Correspondance Course - Lesson 24

Somo la 24

KWA NEEMA MMEOKOLEWA

SOMO: Warumi 5

NEEMA

Katika Biblia neema ya Mungu maana yake ni wema wa upendo wa Mungu kwa wanadamu. Ni kitu asichokistahili mtu, na ni zawadi ya bure kabisa inayotoka kwake. Neema hiyo inaeleweka vizuri zaidi katika kumtoa Bwana Yesu kwa ajili ya kutuokoa.

(Utahitaji kulikumbuka hili vizuri unavyojifunza somo hili)

Correspondance Course - Lesson 22

SOMO LA 22

DHAMBI NA MATOKEO YAKE (SEHEMU YA 1)

SOMO: Mwanzo 2 na 3

Dunia iko katika hali mbaya: vita, njaa, magonjwa, vurugu, mauaji, mateso n.k. Lakini, Mungu aliiumba dunia ikiwa ‘njema’. Mwanadamu ameichafua! Hulka ya mwanadamu ya uchoyo, ubinafsi, wivu na kutotii-mamlaka vimeiharibu jamii na dunia hii.

Yalianzia wapi ‘kwenda mrama’?

Hapo mwanzo Mungu alimuumba mwanadamu wa kwanza, Adamu. Adamu aliumbwa kutokana na mavumbi ya nchi:

Correspondance Course - Lesson 21

Somo la 21

KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU

SOMO:  Matendo 8

Yesu aliwaahidi wanafunzi wake kuwa wangepewa Roho Mtakatifu. Aliwaambia:

“Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo, watasema kwa lugha mpya, watashika nyoka, hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa, wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya” (Marko 16:17,18).

Correspondance Course - Lesson 20

Somo la 20

ROHO MTAKATIFU WA MUNGU

SOMO:  Marko 1

“Mungu akasema, iwe nuru, ikawa nuru” (Mwanzo 1:3). Inaonekana kama rahisi sana. Lakini hebu ifikirie hiyo nguvu kubwa ya kiutambuzi na kiuweza iliyohitajika, kabla hiyo nuru haijaweza kupatikana:

“Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi” (Mwanzo 1:1).

Correspondance Course - Lesson 18

Somo la 18

KIFO CHA YESU

SOMO: Marko 14 na 15

Tatizo la Dhambi
Ni dhahiri kuwa, dhambi ni janga kubwa kwa mwanadamu. Ni tatizo ambalo hata mtu anayeonekana mkweli sana, anashindwa kulitatua. Hakuna mtu anayeweza kuishinda dhambi kwa jitihada zake mwenyewe. Biblia yote inahusu namna Mungu alivyotoa jawabu kwa tatizo hili.

Maisha ya Yesu - Somo la 17

Somo la 17

MAISHA YA YESU

SOMO:  Luka 2

“Malaika akamwambia, usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yesu. Huyu atakuwa mkuu, ataiwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Atamiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho” (Luka 1:30 – 33).

Baba na Mwana - Somo la 16

Somo la 16

BABA NA MWANA.

SOMO: Isaya 45

“Je! Wewe waweza kuuvumbua ukuu wa Mungu?” (Ayubu 11:7)

Hili swali liliulizwa maelfu ya miaka iliyopita. Jibu lake ni lile lile leo kama lilivyokuwa kwa siku hizo; kwa vyovyote hatuwezi! Hakuna kitu kabisa tunachoweza kujua kumhusu Muumbaji Mkuu wa vitu vyote, nje ya yale Yeye Mwenyewe anayotuambia katika Neno lake; katika Biblia. Hata hivyo hakuna tumaini la uzima wa milele tunaloweza kulipata, bila ya huko kumjua.

Ahadi za Mungu kwa Daudi - Somo la 15

Somo la 15

AHADI ZA MUNGU KWA DAUDI

Somo: 2 Samweli 7

Kijana mchunga-kondoo awa mfalme

Utakuwa pengine umesikia juu ya Daudi, kijana aliyekuwa mchungaji wa kondoo, aliyemuua Goliati, mtu wa ‘maraba mitatu’ kwa kijiwe kimoja alichomtupia.

Daudi aliishi kama miaka 1000 kabla ya Yesu Kristo kuzaliwa. Alizaliwa katika eneo moja na Yesu, katika mji mdogo karibu na Yerusalemu uitwao Bethlehemu. Alikuwa mwana wa kiume wa mwisho wa Yese, aliyekuwa mmiliki wa hao kondoo.