CSSA 1-3-08 - ELIJAH AND THE STILL SMALL VOICE

58. ELIYA NA SAUTI NDOGO YA UTULIVU

“Sauti ikamjia, kusema, Unafanya nini hapa, Eliya?”

 

Shabaha

Kuonyesha namna Eliya alivyojifunza kutokana na sauti ndogo ya utulivu kwamba Mungu bado alikuwa na kazi ya kufanya katika Israeli. Huko katika mlima wa Karmeli, Mungu alikuwa amewaonyesha Waisraeli kwa njia ya ajabu kwamba yeye ndiye alikuwa Mungu wa kweli na ya kwamba hakuna Mungu mwingine. Kwa hakika sasa wangemtumikia Mungu na kuzishika amri zake.

 

CSSA 1-3-07 - THE CONTEST ON MOUNT CARMEL

57. MASHINDANO KATIKA MLIMA KARMELI

“BWANA akiwa ndiye Mungu, mfuateni; bali ikiwa Baali ni mungu, mfuateni yeye”

 

Shabaha

Kuonyesha namna Mungu alivyothibitisha kwa watu mlimani Karmeli kwamba yeye ndiye alikuwa Mungu wa kweli na aliye hai. Ukame uliendelea katika Israeli kwa muda wa miaka mitatu na nusu (Luka 4:25) Nchi ilikuwa kame na ilikuwa imekauka kabisa.

 

CSSA 1-3-06 - ELIJAH THE PROPHET

56. NABII ELIYA

“Hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, mpaka kwa neno langu”

 

Shabaha

Kuonyesha jinsi Mungu alivyoleta ukame juu ya nchi lakini akamtunza Eliya na kumbariki mwanamke mjane wa Sarepta kwa ajili ya wema wake kwa Eliya. Ufamle wa kaskazini wa Israeli ulianza vibaya sana. Kama tulivyoona, kitu cha kwanza ambacho Yeroboamu alifanya kilikuwa kubadili ibada ya kweli ya Mungu kwa kuabudu miungu (sanamu). Alipoondoka Mfalme mwovu mwingine Mfalme mwovu aliifuata.