Correspondance Course - Lesson 10

Somo la 10

MUNGU  ANAVYOIONA  HISTORIA

SOMO: Danieli  2

Mungu hatazami historia kwa namna tunavyoitazama sisi. Ile watu wanayoiona kama dola yenye nguvu sana, inaweza kuwa si chochote machoni pake. Kwa upande mwingine, mtu anayeonekana mkimya, mwenye unyonge, anayedharauliwa na wenzake, anaweza kuwa wa thamani kubwa machoni pa Mungu.

Correspondance Course - Lesson 09

Somo la 9

UFALME WAKO UJE

SOMO : 1 Nyakati 29

“Ufalme wako uje. Mapenzi yako yatimizwe hapa duniani kama mbinguni”.

Ni mara ngapi umeyasema maneneo haya, au kuyasikia yakitamkwa na wengine? Yapo yakiwa ni sehemu ya maombi, ambayo Yesu aliwafundisha wanafunzi wake. Unaweza kuyasoma katika Luka 11:2-4. Tunayafahamu maneno haya vizuri, lakini unajua yanachokimaanisha?

Correspondance Course - Lesson 08

Somo la 8

ISHARA ZA KURUDI KWA YESU

SOMO: Luka 21

Yesu atarudi tena hapa duniani. Biblia inatuambia hili wazi wazi sana, kama tulivyoona katika somo lililopita. Kuja kwake ni sehemu ya mpango wa Mungu kwa dunia yetu. Yesu atakuwa ‘Mfalme wa Wafalme’, akiongoza dunia kutoka katika Kiti chake cha Enzi katika Yerusalemu. Hii ilikuwa ahadi ya Mungu kwa Wayahudi katika Agano la Kale, na ni ujumbe muhimu sana wa Agano Jipya kwa watu wote. Wafuasi wa mwanzo wa Bwana Yesu waliutazamia wakati wa kuja mbeleni, wa:

Correspondance Course - Lesson 07

Somo la 7

KURUDI KWA BWANA YESU DUNIANI

SOMO: Matendo 1

Miaka 2000 iliyopita

Bwana Yesu alisulubiwa miaka elfu mbili iliyopita. Wafuasi wake walivunjika moyo na kuchanganyikiwa. Matumaini yao yote kwake yalivunjika, alivyokuwa amekufa na kulazwa kaburini.

     Siku ya tatu, Yesu alitoka kwenye kaburi lile akiwa hai!     

Lakini:

Correspondance Course - Lesson 06

Somo la 6

MUNGU ALIUPENDA ULIMWENGU

SOMO: Isaya 53

Dunia ina matatizo gani?

Ni kweli kuna matatizo katika dunia tunamoishi. Kila siku tunasikia habari za kutisha za ukatili na vurugu duniani kote, na matishio ya vita. Magonjwa ya ajabu-ajabu yanasambaa kwa haraka, na wengi wanakufa kwa njaa wakati wengine wana chakula kingi zaidi ya mahitaji yao. Wafalme na watawala wengine hawaonekani hasa kuguswa na matatizo ya wale wanaowaongoza.